13 February 2006

Changamoto....Ni nani zaidi?.. Winnie au Graca?




Haya jamani, hivi karibuni nitawaleteeni harakati za maisha ya wanawake wa shoka Graca Machel na Winnie Mandela. Wanawake hawa wawili wana mambo mengi yanayoshabihiana katika harakati zao za maisha. Haya, kabla sijawaleteeni undani wao ninawapa changamoto hii ya kujaribu kumtafuta aliye zaidi ya mwenziye. Haya karibuni nami najiweka sawa.

18 Comments:

At Monday 13 February 2006 at 19:39:00 GMT, Blogger John Mwaipopo said...

Swali gumu kidogo kwani watata uzuri wao au siasa zao. Lakini naweza jaribu kidogo. Kwa uzuri ungeweka picha za umri wao sawa sawa- yaani picha zao wakiwa vigori, twenties, 30s, 40s nk. Kwa picha ulizoweka umempendelea Madikizela.

 
At Monday 13 February 2006 at 20:34:00 GMT, Blogger Mija Shija Sayi said...

Ndugu yangu Mwaipopo nimetafuta mno picha ya Graca akiwa kigoli, na katika zote angalau hiyo ndiyo anaonekana kigoli. Kuhusu shindano hili kwa kweli halina mipaka linagusa nyanja zote kuanzia siasa hadi urembo. Haya tuendelee.

 
At Tuesday 14 February 2006 at 13:37:00 GMT, Blogger Reggy's said...

Kwa urembo, kwangu mimi Winnie namba moja, lakini tuangalia msomo 'uzuri si hoja...' Mandela alimuacha kwa nini? tabia chafu. Huyu mwingine nampendea historia yake, sijua kama kuna mwingine aliyewahi kuolewa na Marais wawili wa nchi Tofauti kama yeye-Samora machel na Mandela. Hivi yawezekana, Mandela alianza naye kabla samora hajafa!

 
At Wednesday 15 February 2006 at 12:09:00 GMT, Blogger mwandani said...

Winnie

 
At Thursday 16 February 2006 at 08:31:00 GMT, Blogger Indya Nkya said...

Kuna tetesi kwamba kabla Machel hajamuoa alikuwa ni mchumba wa Edwardo Mondlane aliyekuwa kiongozi wa FRELIMO alivyofariki Machel akachukua. Halafu kuna habari zisizothibitishwa kwamba wakati Mandela akiwa Gerezani na Machel akiwa hai Machel alikuwa akitembea na Winnie. Lakini yote hayo ni maneno ya watu. Mandela pia bwana Regnald ana historia nzuri ya kuacha wanawake. Huyu aliye naye ni wa tatu

 
At Saturday 18 February 2006 at 14:02:00 GMT, Blogger FOSEWERD Initiatives said...

Graca! analipa sana! ukitaka picha yake tafuta kile kitabu cha picha alikitoa nadhani sir George Kahama sijui kilikwa kina picha za Nyerere au Msiba wa Sokoine! kuna picha moja Graca alikuwa amepozi na mchonga nadhani.....japo nilikuwa bwa mdogo nilimzimia pale pale!

 
At Sunday 19 February 2006 at 10:30:00 GMT, Blogger MICHUZI BLOG said...

natamani kuona picha yako, da'mija, ukizingatia mi ndiye meneja wa sisi tambala, nadhaniwajuanasemanini...

 
At Sunday 19 February 2006 at 18:35:00 GMT, Anonymous Anonymous said...

Da Mija, unaweza kumwambia Graca apunguze ukubwa wa mawani yake? Nadhani mawani yale huwa yanampunguzia maksi. Au?
Ngoja nifikirie nani zaidi...hivi ni kiitikadi, kikazi, kisura, au vyote?

 
At Sunday 19 February 2006 at 21:56:00 GMT, Blogger John Mwaipopo said...

Michuzi tazama kapicha ka Da'Mija kunako albamu yake hapo kwenye viunganishi. Yuko 'Bomba Mbaya' babake!

 
At Sunday 19 February 2006 at 21:59:00 GMT, Blogger John Mwaipopo said...

Naona keshakitoa kiugnanishi cha 'alibamu' yake

 
At Monday 20 February 2006 at 16:26:00 GMT, Anonymous Anonymous said...

Miye wangu Winnie! Maelezo zaidi baadaye.

F MtiMkubwa Tungaraza.

 
At Monday 20 February 2006 at 21:40:00 GMT, Blogger boniphace said...

Kwa staili ya picha hizi mimi sisemi maana domo lilianza kubaki kimya, nikatazama chini na kuchimba sakafu. Nikatupa tena jicho katika skirini ya kompyuta yangu na mwisho nikakuza picha hiyo full skrini. Bado sikuridhika nikaona niiweke kwenbye CD ili nikaprinti kabisa na kuitunza. Lakini baadaye nikagundua nilikuwa naota tu...kweli Mija sina hali wala mali. Kwendako Hisani hakurudi Nuksani, nipe siku nitasemea Kasrini kwangu.

 
At Tuesday 21 February 2006 at 12:19:00 GMT, Blogger Reggy's said...

Inda nataka uthibitishe kuwa mimi ninaacha wanawake na niliye naye ni tatu

 
At Tuesday 21 February 2006 at 20:40:00 GMT, Blogger John Mwaipopo said...

Swali zuri Reginald.

 
At Tuesday 21 February 2006 at 21:56:00 GMT, Blogger Mija Shija Sayi said...

Kama nimemuelewa vizuri bwana Idya, si kwamba anasema bwana Miruko ana mke wa tatu sasa, ila anamueleza bwana Miruko kwamba, kwa Mandela huyu ni mke wa tatu na si wapili kama wengi wanavyojua.

Sijui kama niko sawa, kama siko sawa basi Idya inabidi uthibitishe tamko lako.....

 
At Friday 24 February 2006 at 14:58:00 GMT, Blogger Indya Nkya said...

Da Mija upo sahihi kabisa namweleza Mandela na si Miruko.

 
At Saturday 25 February 2006 at 11:01:00 GMT, Blogger FOSEWERD Initiatives said...

wajameni! kwa taarifa yenu! yule bwa mdogo alikuwa anamsaidia mandela wakati amefungwa na kujichana michuzi ya ANC na maza hivyo kupelekea kuvunjika kwa ndoa ya winnie na mandela anaitwa Dali Mpofu na sasa ni CEO wa South African Broadcast Coorporation! SABC. wakati huo kijamaa kilikuwa kikoo varsity! - inawezekana kabisa msaada huu alioutoa ndio umempa kapost!haya mambo bwana!

 
At Sunday 26 February 2006 at 11:40:00 GMT, Blogger MICHUZI BLOG said...

mnaniruhusu kuwahamishia kwangu ili niweke picha latest ya mandela akiwa na wote wawili hivi karibuni? we mwaipopo usipotoshe umma. utajaji vipi kwa picha za zamani. halafu ndesanjo usivunge. jibu unalo. ugonjwa wako kwa kinamama naujua, ingawa ntakuachia useme mwenyewe kabla sijakuumbua.

 

Post a Comment

<< Home