Wadau na wanablogu wote kwa ujumla, nina furaha kuwapasha habari kwamba mwezi uliopita June 10 2008, Nilipata mtoto wa kike anayekwenda kwa jina la Manjula. Manjula anaendelea vizuri na muda si mrefu na yeye atajiunga katika ulimwengu wa ku-blogu anaomba baraka zenu wadau.
13 July 2008
Baby Manjula huyu hapa...
Wadau na wanablogu wote kwa ujumla, nina furaha kuwapasha habari kwamba mwezi uliopita June 10 2008, Nilipata mtoto wa kike anayekwenda kwa jina la Manjula. Manjula anaendelea vizuri na muda si mrefu na yeye atajiunga katika ulimwengu wa ku-blogu anaomba baraka zenu wadau.
29 April 2008
Filamu zinazowania tuzo ya Vinara wa Filamu Tanzania zatajwa
Filamu zilizoingizwa na watengenezaji wa filamu nchini kuwania tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania 2007/2008 2007/2008 (Vinara Film Awards), zimetajwa.
Katika taarifa kutoka mratibu wa One Game Promotion inayoaandaa tuzo hizo, Khadija Khalili, iliyotumwa kwenye vyombo vya habari zaidi ya filamu sabini zinawania tuzo hizo.
Taarifa hiyo ilizitaja filamu hizo kuwa ni Crying Silently (Kilio Moyoni), Kolelo, Mwanahiti, Zawadi ya Fisadi, Oloboni na Layoni, Mmera (Jando) na Nyamaume.
Nyingine ni Sumu ya Moyo, Segito, A Point of no Return I, A Point of no Return II, Dar to Lagos, Cross my Sin na Penina.
Pia zimo Habari Kubwa, Fake Pastor, Chite Ukae, Surprise, Stranger, Fungu la Kukosa, Sea Man, Mzee wa Chabo, Donda Ndugu, I Love You, Miss Bongo I, Miss Bongo II, Revenge, Behind the Scene, na My Wife.
Taarifa hiyo ilizitaja nyingine kuwa ni My Sisters I, My Sisters II, Machozi ya Nyamoma, Silent Killer, My Wife, Greena, Kiapo cha Damu, Valentine, Mwana Pango, Utata, Yolanda, Picnic, Uwanja wa Dhambi, Misukosuko II, Copy, Lugha Gongana, Mtoto wa Mjini, Nyuma ya Pazia, Macho Mekundu, Tanzia, Welcome Back, Karibu Paradiso, Swahiba, The Game of Love I, The Game of Love II na The Game of Love III.
Nyingine ni Mahabati, Security, Itunyama, The Body Guard, Agano la Urithi, Ndani ya Gereza, Simu ya Kifo, My Heart, Malipo ya Kisasi I, Malipo ya Kisasi II, Mpasuko wa Moyo I, Mpasuko wa Moyo II, Kisasi na Diversion of Love.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa, majaji watakutana wiki ijayo kuanza kuziangalia tuzo hizo.
Taarifa hiyo ilisema kuwa filamu zinazowania tuzo hizo ni zile zilizokamilika kutengenezwa Januari 2007 mpaka Machi 31, 2008.
Vipengele vinavyoangaliwa na majaji katika filamu hizo ni Filamu Bora ya Mwaka, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kike, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kike, Muongozaji Sinema Bora wa Mwaka, Mchekeshaji Bora wa Mwaka, Mwandishi Bora wa Filamu na Mtunzi Bora wa Filamu.
Vingine ni Filamu Bora ya Kutisha, Muigizaji Mwandamizi Bora wa kike (supporting actor), Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kike, Adui Bora kwenye Filamu, Wimbo Bora wa Mwaka (Sound Track), Mhariri Bora wa Filamu ambao wote watapata tuzo na zawadi.
Pia itatolewa tuzo ya heshima kwa wale waliotoa mchango wao kukuza sanaa nchini.
Tuzo hizo zinazotarajiwa kutolewa mwishoni mwa mwezi Mei zimedhaminiwa na bia ya Ndovu Special Malt, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Global Publishers
Katika taarifa kutoka mratibu wa One Game Promotion inayoaandaa tuzo hizo, Khadija Khalili, iliyotumwa kwenye vyombo vya habari zaidi ya filamu sabini zinawania tuzo hizo.
Taarifa hiyo ilizitaja filamu hizo kuwa ni Crying Silently (Kilio Moyoni), Kolelo, Mwanahiti, Zawadi ya Fisadi, Oloboni na Layoni, Mmera (Jando) na Nyamaume.
Nyingine ni Sumu ya Moyo, Segito, A Point of no Return I, A Point of no Return II, Dar to Lagos, Cross my Sin na Penina.
Pia zimo Habari Kubwa, Fake Pastor, Chite Ukae, Surprise, Stranger, Fungu la Kukosa, Sea Man, Mzee wa Chabo, Donda Ndugu, I Love You, Miss Bongo I, Miss Bongo II, Revenge, Behind the Scene, na My Wife.
Taarifa hiyo ilizitaja nyingine kuwa ni My Sisters I, My Sisters II, Machozi ya Nyamoma, Silent Killer, My Wife, Greena, Kiapo cha Damu, Valentine, Mwana Pango, Utata, Yolanda, Picnic, Uwanja wa Dhambi, Misukosuko II, Copy, Lugha Gongana, Mtoto wa Mjini, Nyuma ya Pazia, Macho Mekundu, Tanzia, Welcome Back, Karibu Paradiso, Swahiba, The Game of Love I, The Game of Love II na The Game of Love III.
Nyingine ni Mahabati, Security, Itunyama, The Body Guard, Agano la Urithi, Ndani ya Gereza, Simu ya Kifo, My Heart, Malipo ya Kisasi I, Malipo ya Kisasi II, Mpasuko wa Moyo I, Mpasuko wa Moyo II, Kisasi na Diversion of Love.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa, majaji watakutana wiki ijayo kuanza kuziangalia tuzo hizo.
Taarifa hiyo ilisema kuwa filamu zinazowania tuzo hizo ni zile zilizokamilika kutengenezwa Januari 2007 mpaka Machi 31, 2008.
Vipengele vinavyoangaliwa na majaji katika filamu hizo ni Filamu Bora ya Mwaka, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kike, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kike, Muongozaji Sinema Bora wa Mwaka, Mchekeshaji Bora wa Mwaka, Mwandishi Bora wa Filamu na Mtunzi Bora wa Filamu.
Vingine ni Filamu Bora ya Kutisha, Muigizaji Mwandamizi Bora wa kike (supporting actor), Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kike, Adui Bora kwenye Filamu, Wimbo Bora wa Mwaka (Sound Track), Mhariri Bora wa Filamu ambao wote watapata tuzo na zawadi.
Pia itatolewa tuzo ya heshima kwa wale waliotoa mchango wao kukuza sanaa nchini.
Tuzo hizo zinazotarajiwa kutolewa mwishoni mwa mwezi Mei zimedhaminiwa na bia ya Ndovu Special Malt, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Global Publishers
30 March 2008
FOMU ZA TUZO ZA VINARA ZATOLEWA.
Fomu za ushiriki katika kinyang'anyiro cha kuwania Tuzo za Vinara wa
filamu Tanzania 2007/8 zimeanza rasmi kutolewa jana katika vituo
mbalimbali nchini ikiwa ni hatua ya kwanza kabla ya kutolewa kwa tuzo
hizo.
Tuzo hizo zitakazotolewa kwa mara ya kwanza nchini, zimeandaliwa na
kampuni ya One Game Promotions na kudhaminiwa na Kampuni ya Bia
Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya dovu Power Malt.
Mratibu tuzo hizo, Khadija Khalili, amesema kuwa, kutokana na sababu
zilizo nje ya uwezo wao, fomu hizo zilichelewa kutoka kwa tarehe ya
awali hivyo kusababisha kuongezwa kwa muda wa kurejeshwa fomu na
kupokea filamu zitakazoshiriki katika tuzo hizo hadi Aprili 18 badala
ya Machi 31 kama ilivyotangazwa awali.
Alisema watengenezaji wa filamu nchini wanakaribishwa kutuma nakala za
filamu zilizotengenezwa kati ya Januari 2007 hadi Machi 31, 2008, kwa
ajili ya kuwania tuzo hizo.
Khalili alisema kuwa, jopo la majaji litakutana baada ya Aprili 18
kuchagua watakaowania tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania 2008.
Alisema fomu za kushiriki kuwania tuzo hizo zinapatikana katika vituo
vilivyotangazwa awali ambavyo ni ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa
(BASATA) kwa Omari Mayanga, pia zinapatikana kwa wasambazaji wa filamu
ambao ni Wananchi Wote, GMC, Kapico na Game First Quality.
"Fomu zilizojazwa na nakala ya filamu iliyopo kwenye mfumo wa VCD na
DVD zitumwe kwenye ofisi za BASATA zilizopo Ilala Bungoni jijini Dar
es Salaam au ofisi ya One Game Promotion," alisema.
Vipengele vitavyoangaliwa na majaji katika filamu hizo kuwa ni Filamu
Bora ya Mwaka, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora wa
Mwaka wa Kike, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji
Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kike, Mwongozaji Sinema Bora wa Mwaka,
Mchekeshaji Bora wa Mwaka, Mwandishi Bora wa Filamu, Mtunzi Bora wa
Filamu, Filamu Bora ya kutisha, Muigizaji Mwandamizii Bora wa kike
(supporting actor), Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kike, Adui Bora
kwenye Filamu, Wimbo Bora wa Mwaka (Sound Track), Mhariri Bora wa
Filamu ambao wote watapata tuzo na zawadi. Pia itatolewa tuzo ya
heshima kwa wale waliotoa machango wao kukuza sanaa nchini.
filamu Tanzania 2007/8 zimeanza rasmi kutolewa jana katika vituo
mbalimbali nchini ikiwa ni hatua ya kwanza kabla ya kutolewa kwa tuzo
hizo.
Tuzo hizo zitakazotolewa kwa mara ya kwanza nchini, zimeandaliwa na
kampuni ya One Game Promotions na kudhaminiwa na Kampuni ya Bia
Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya dovu Power Malt.
Mratibu tuzo hizo, Khadija Khalili, amesema kuwa, kutokana na sababu
zilizo nje ya uwezo wao, fomu hizo zilichelewa kutoka kwa tarehe ya
awali hivyo kusababisha kuongezwa kwa muda wa kurejeshwa fomu na
kupokea filamu zitakazoshiriki katika tuzo hizo hadi Aprili 18 badala
ya Machi 31 kama ilivyotangazwa awali.
Alisema watengenezaji wa filamu nchini wanakaribishwa kutuma nakala za
filamu zilizotengenezwa kati ya Januari 2007 hadi Machi 31, 2008, kwa
ajili ya kuwania tuzo hizo.
Khalili alisema kuwa, jopo la majaji litakutana baada ya Aprili 18
kuchagua watakaowania tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania 2008.
Alisema fomu za kushiriki kuwania tuzo hizo zinapatikana katika vituo
vilivyotangazwa awali ambavyo ni ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa
(BASATA) kwa Omari Mayanga, pia zinapatikana kwa wasambazaji wa filamu
ambao ni Wananchi Wote, GMC, Kapico na Game First Quality.
"Fomu zilizojazwa na nakala ya filamu iliyopo kwenye mfumo wa VCD na
DVD zitumwe kwenye ofisi za BASATA zilizopo Ilala Bungoni jijini Dar
es Salaam au ofisi ya One Game Promotion," alisema.
Vipengele vitavyoangaliwa na majaji katika filamu hizo kuwa ni Filamu
Bora ya Mwaka, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora wa
Mwaka wa Kike, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji
Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kike, Mwongozaji Sinema Bora wa Mwaka,
Mchekeshaji Bora wa Mwaka, Mwandishi Bora wa Filamu, Mtunzi Bora wa
Filamu, Filamu Bora ya kutisha, Muigizaji Mwandamizii Bora wa kike
(supporting actor), Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kike, Adui Bora
kwenye Filamu, Wimbo Bora wa Mwaka (Sound Track), Mhariri Bora wa
Filamu ambao wote watapata tuzo na zawadi. Pia itatolewa tuzo ya
heshima kwa wale waliotoa machango wao kukuza sanaa nchini.
13 March 2008
Je serikali inalichukuliaje hili?..

Wadau naomba tuisome habari hii hapa halafu tujadili je serikali ina mpango gani hasa juu ya maalbino? kwa sababu hadi sasa hivi bado sijaona hatua yoyote inayochukuliwa, hivi jamani ni haki wanayofanyiwa wenzetu?
22 February 2008
Kazi mpya za Msanii Hendrix Lilanga.




Msanii mchoraji maarufu anayeendeleza kazi za babu yake, Hendrix Lilanga ametuletea kazi zake mpya za kufungua mwaka. Hendrix amefungua pia ukurasa wa kazi zake katika mtandao wa picha wa flickr, mtembelee ujionee mwenyewe mambo yake. Anuani yake ya barua pepe bado ni ileile hendrylilanga@yahoo.com au unaweza kuwasiliana nami kwa maelezo zaidi juu ya kazi zake tumia dadamija@yahoo.com
21 February 2008
Hongera kwa siku ya kuzaliwa 21/02.

Leo mzee Mugabe na mwanangu wanaadhimisha siku zao za kuzaliwa, sasa huwa najiuliza sijui na bibie atakuwa na msimamo kama wa babu?, jibu sipati. Lakini yote maisha cha maana Mungu awazidishie maisha marefu. Happy birthday wooote waliozaliwa siku hii.
20 February 2008
Unawafahamu African Mama's?

Basi kama hauwafahamu au hata kama unawafahamu basi jaribu kuwapitia hapa halafu utaniambia mwenyewe kama si wanawake wa shoka hawa.
Je unataka kuwa wa shoka? Fuatilia vidokezo hapo chini.

Wataalamu wanasema kuwa mtu wa shoka si lelemama, inahitaji nidhamu ya hali ya juu katika uendeshaji wako wa maisha ya kila siku. Kwanza kabisa wanakuambia THINK BIG! Endelea msomaji...
Talent: Our Creator has endowed all of us not just with the ability to
sing, dance or throw a ball, but with intellectual talent. Start
getting in touch with that part of you that is intellectual and
develop that,
and think of careers that will allow you to use that.
Honesty: If you lead a clean and honest life, you don't put skeletons
in the closet. If you put skeletons in the closet, they definitely
will
come back just when you don't want to see them and ruin your life.
Insight: It comes from people who have already gone where you're trying
to go. Learn from their triumphs and their mistakes.
Nice: If you're nice to people, then once they get over the suspicion
of why you're being nice, they will be nice to you.
Knowledge: It makes you into a more valuable person. The more knowledge
you have, the more people need you. It's an interesting
phenomenon,
but when people need you, they pay you, so you'll be okay in
life.
Books: They are the mechanism for obtaining knowledge, as opposed to
television.
In-Depth Learning: Learn for the sake of knowledge and understanding,
rather than for the sake of impressing people or taking
a test.
God: Never get too big for Him.
19 February 2008
Wamama..

Hivi ule usemi usemao mafanikio ya mwanaume kwa kiwango kikubwa huchangiwa na mwanamke, ikiwa na maana mkewe ni wa kweli? na kama ni wa kweli je wake za viongozi nao wanaweza kuwekwa katika kundi la wanawake wa shoka?
Nawauliza wadau swali hili kwa vile nimekuwa nikijiuliza sana kama wake wa viongozi ni wanawake wa shoka au vinginevyo. Tusaidiane jamani.
29 November 2007
03 November 2007
Sanaa ya George lilanga chini ya mrithi hendrix Lilanga.
Pichani ni mimi na Msanii Hendrix lilanga.
Hapo awali nilitoa changamoto ya picha ya sanaa na kuwataka wadau wangu kumtambua mwanzilishi wake. Wadau mmejitahidi lakini bahati mbaya jibu sahihi halikuweza kupatikana. Leo napenda kutoa jibu la swali lile. Sanaa ile ni ya mkongwe marehemu GEORGE LILANGA, lakini imechorwa na Mjukuu wake mkubwa ndugu Hendrix Lilanga ambaye pia ndiye mrithi wa shughuli zote alizokuwa akifanya babu yake.
Nilibahatika kukutana na Hendrix Lilanga hivi karibuni, tuliongea mengi ikiwa ni pamoja na mikakati aliyoiweka katika kutaka kuiendeleza kazi ya babu yake. Kwa kifupi alinieleza kwamba yeye alizaliwa Tegeta mkoa wa Dar es Salaam tarehe 20/10/1974.
Alipata elimu yake ya msingi mkoani Tanga, lakini hakuweza kuendelea na masomo ya sekondari kutokana na matatizo ya kifamilia. Ndipo mwaka 1993 babu yake aliamua kumuingiza rasmi mjukuu wake katika shughuli za sanaa aliyokuwa akiifanya. Mzee Lilanga alimfundisha shughuli
1. Kuchora Oil Painting katika Carnivals, Hard Boad
2. Water Colour Painting katika Karatasi
3. Batick Picture
4. Goat Skin Drawings
5. Vibuyu ( Callabash Drawings)
Hendrix hakuishia hapo, Mwaka 2007 alihudhuria course ya Graphic katika Chuo cha Enternational Summer Academy Salzburg kilichoko Austria.
Kwa upande wa maonesho ameshafanya maonesho yafuatayo:-
1. Bagamoyo Arts Festival mwaka 1999 Tanzania
2. Art in Tanzania mwezi 11 mwaka 2000
3. Art in Tanzania mwezi 11 mwaka 2001
4. Real Art Gallery mwezi 7 mwaka 2006 Zanzibar
5. Tanart Enterprises mwezi 6 mwaka 2007 Dar es Salaam Tanzania
6. International summer Academy, mwezi 8 mwaka 2007 Salzburg Austria.
Kwa sasa anaendelea na shughuli za sanaa za michoro na kufundisha wasanii chipukizi mbinu mbali mbali katika mambo ya sanaa kwa ujumla. Yuko mbioni kutengeneza website yake ili watu wengi waweze kufaidika na michoro ya sanaa afanyazo. Na anapatikana kwa anuani hii hendrylilanga@yahoo.com
Ajali barabarani nchini....na Born again Pagan
Nimepokea maoni maridhawa kutoka kwa baba yetu mpendwa BAP, hebu tuyasome na kujadili kimapana anayosema, endelea ndugu msomaji...
Hivi karibuni, katika mojawapo ya blogu nyingi mashuhuri za wa-Tanzania, niliahidi kwa kuwaomba wanakijiji kujipa muda wa tutafakuri na kuchangia suala la ajali barabarani na jinsi ambavyo tunaweza kupunguza “balaa” hili ambalo linaendelea kutusibu siku hadi siku, mchana na usiku.
Ingawa ni wanakijiji kama wawili hivi walichangia, sikukata tamaa.
Nazidi kuwaombeni tujaze blogu hizi kwa maoni yetu kuhusu maafa ya ajali barabarani. Blogu hizi zinasomwa na wengi, wakiwemo viongozi wa serikali, wabunge wetu, viongozi wa dini na mashirika yasiyo ya serikali.
Napenda kurudia mchango wangu wa awali kuhusu ajali nchini mwetu, ikiwa ni sehemu ya maombolezo ya kutokwa na Naibu Waziri Salome Mbatia. Mhariri wa gazeti maarufu nchini la kila siku aliandika, “…taifa limeghubikwa na majonzi makubwa kufuatia kifo (cha Naibu Waziri Salome Mbatia) kilichotokana na ajali ya gari eneo la Kibena, Njombe mkoani Iringa Alhamisi.”
Lakini yatubidi kuzingatia kwamba si Salome Mbatia peke yake aliyekufa katika ajali hiyo. Dereva wake na utingo wa lori nao walikufa.
Na sio ajali hiyo tu iliyotokea siku hiyo na kusababisha mauaji! Karibu watu kama kumi hivi walikufa kwa ajali barabarani siku hiyo! Lakini kifo cha Naibu Waziri Salome Mbatia kimepewa kipaumbele zaidi ya vifo vya wengine. Sababu zinaeleweka; sina haja ya kuzirudia.
Mhariri huyo alitoa tahadhari kali kuitaka “Serikali na vyombo husika na sekta ya usafirishaji” kudhibiti ajali: “[Y]afaa tatizo hili la ajali za barabarani zinazotokana na uzebe na mwendo wa kasi litizamwe tena kwa makini.
Bado linapoteza maisha ya watu wengi wasio na hatia wakati zinaweza kuepukwa. Madereva wengi bado wamekuwa ni vichwa maji katika uendeshaji wao barabarani.”
Kauli kama hiyo ya mhariri, sambamba na kauli nyingi za umma zisizotangazwa, inaitaka serikali yetu kamwe isingoje “kifo cha mzaliwa wa kwanza”, kama mtawala Firauni wa Misri, ndipo iamke na kufanya lolote dhidi ya “janga” hili ambalo hudonoa maisha ya wa-Tanzania wetu!
Tumezoea kusema, “Ajali haina kinga!” Lakini ukweli ni kwamba ajali inaweza ikakingika!
Wengine husema, “Ngoja ajali ziwamalize kwa kumwonea Kabwe Zubeir Zitto!”
Hili nitalizungumzia kwa kifupi:
Katika magazeti na blogu nyingi kumeibuka tabaka la washirikina au niwaite “wanajimu wabaya, watabiri mabaya, wenye ndoto mbaya, wenye maono” wenye kungojea “kiyama” kiikumbe serikali na CCM yake.
Wenzetu wanamwomba m-Bunge wetu “kijana” Zitto Zubeir Kabwe aombe miungu ya huko kwao Kigoma kuweka breki ili isiwamalize wote wale waliomnyoshea kidole - mizimu ya Kigoma inalipa kisasi!
Wanaoanisha msululu wa ajali ambazo zimetokea kwa baadhi ya viongozi wa CCM kufuatia mzozo wa m-Bunge wetu “kijana” Zitto Zubeir Kabwe eti zinatokana na “kumwonea Zitto”!
Natarajia kuchangia hili la mzozo wa Zitto, kulingana na maoni ya wasomi wetu wawili: Prof. Gidion Shoo (Zitto Hakuwatendea Mema Wananchi,” kwa mujibu wa “Kanuni za Bunge”. Msomi mwingine ni Prof. Shivji (Zitto Kabwe’s Suspension an Episode or an Epitah?)
Kero ya Zitto yaonyesha jinsi ambavyo nchi yetu imejigawa. Kuna ukweli kwamba wote hatuimbi, “Tanzania, Tanzania, nakupenda kwa moyo wote; nilalapo nakuota, jina lako ni tamu sana”!
Ni lazima kuna sababu zake, mbali ya vitendo vya rushwa na ufisadi!
Kuna baadhi yetu ambao wamegeuka washirikina na kuonyesha hali ya chini kabisa. Hawa wanaomba mabaya zaidi yawapate wana-CCM, kwa jumla, na hasa wale viongozi waliojeruhiwa katika ajali mbali mbali!
Sioni kama hili ni ombi la kiungwana! Ni matakwa ya wendawazimu kwani endapo CCM inafanya mabaya, kuitakia mabaya nako ni vibaya! Makosa mawili hayajengi au hayazai haki!
Kumtakia mwenzako kifo ni sawa na kumwua tu. Leo tunatakiana vifo; kesho tutauana kimacho macho!
Kuna wengine wenye kuamini kuwa ajali “Ni mipango ya Mungu - Mungu kapenda; siku yako ya kufa ikifika, imefika!”
Hili pia yanataka ufafanuzi:
Je, maisha yetu yamewekewa
“blinkers” za “determinism”? Je, hakuna lolote tunaloweza kufanya kuepusha hiyo “determinism”? Mbona tunataka kuingilia kati nguvu za asili (nature) kwa kualika nchini “wachawi wa mvua” kutoka Thailand?
Maisha yanajengeka kutokana na kuoana kwa akili zetu na maingilio ya mazingira tuliyomo. Tunaweza kuyabadili kwa kupata elimu tosheleza na hekima ya kuweza kutafukari na kutafuta njia za kusuluhisha au kutanzua tatizo la ajali barabarani.
Wengine, hasa wadini walokoke huamini kuwa Mungu huadhibu kwa sababu ya dhambi. Hii sio kwa wa-Tanzania tu bali pia wahubiri wengi walokoke duniani, hususani, Marekani.
Mhubiri mmoja mlokoke wa Amerika aliwahi kutamka kuwa Jimbo la Florida lilipatwa na madhara ya kuwaka moto kutokana na dhambi za kisenge na kishoga.
Mlokoke huyo huyo alimshutumu Waziri Mkuu wa Israel kwa kupatwa na mshituko uliomlemaza kuwa ni kwa sababu kagawa nchi ya Palestine - nchi ya Mungu - kwa Wapalestina!
Kisa kingine cha hivi karibuni: Jaji wa “federal” hapa Amerika ameamuru kanisa moja la Ki-Baptist la Westboro - kanisa lenye kuhubiri na kueneza chuki - kulipa faini ya dola millioni 10.9 kwa kushangilia kifo na kukielezea kifo hicho cha askari Lance Cpl Matthew Snyder vitani Iraq Machi 2006 kuwa ni adhabu kutoka kwa Mungu.
Washirika walokoke wengi wa hapa Amerika wanahubiri ‘injili ya chuki” dhidi ya ushoga na kubagua mazishi ya watu waliokufa kwa ukimwi. Walokole wengine wanaamini kuwa Amerika inapata majanga, kama hilo la 911, kwa sababu wameacha kumcha Mungu!
Je, Mungu anatuadhibu na hizo ajali zitokeazo barabarani?
Pengine hilo la ajali na kudra za Mwenyenzi Mungu nalo linahitaji muda wake maalum wa kutafukari kwa undani, hasa kwa wale wenye kutaka kujua kutoka kwa wanaolielewa vizuri.
Kuna baadhi yetu wenye kuziona na kuzitafukari ajali barabarani na kwinginepo, kama matukio ya kawaida tu. Tusitekwe nyara na fikra za kufungwa macho yetu na akili zetu kuamini kwamba ajali haina kinga; ajali ni adhabu ya Mungu, au ni matakwa mengine ya ushirikina. Ajali husababishwa na/au mchanganyiko wa haya matatu:
dereva, gari na barabara.
Kuna Ripoti ya Mwaka 1994 inayoelezea rasmi na kwa undani kuhusu usafiri nchini. Sijui ni wangapi kati ya matrafiki husika, wamiliki wa magari, maderera na abiria wa kawaida wameipitia ripoti hii?
Kuna vitu vitatu muhimu katika njia za usafiri wa nchi kavu kwa kutumia magari barabarani: dereva, gari na barabara. Kila kimoja kina masharti yake sawa na “social environment”: mshiriki (actor/participant), kusudi (purpose), sheria (rules and regulations), mipaka (boundaries), maadili (morality), siasa (what is to be done), na lugha (technical language).
Dereva: Kulingana na Ripoti hiyo, sababu kubwa ya ajali nchini mwetu hutokana na madreva wenyewe. Ajali za namna hii ni kiasi cha asilimia 76.
Napenda kuongezea kuwa u-mahiri na u-makini wa kuendesha unatokana na mafunzo tosheleza na utahini usiopendelea; dereva kujiandaa vya kutosha kabla ya safari; asiendeshe huku amelewa au amechoka; afuate sheria za barabarani; na uwezo wa dereva kubaini endapo gari lake lina udhaifu au kasoro.
Ajali nyingi za mabasi, malori yetu na magari madogo yetu kugongana vichwa kwa vichwa, kama ajali hiyo iliyotokea na na kuchukua maisha ya wakina Waziri Mbatia, dereva na utingo wa lori.
Hii ina maana kuwa sababu kubwa ni pale dereva wa gari linalofuata kutaka ku-“overtake” lililotangulia karibu na mwisho wa kilima au kwenye kona kali bila kujua kuwa kuna gari lingine linakuja mbele.
Wakati mwingine gari hupata kasoro na dereva kushindwa kuliongoza. Sababu nyingine ni kwa dereva kuchoka na kusinzia sinzia na mwisho kupoteza saiti yake.
Madereva wengine huendesha kulingana na wimbo wa mapenzi wa Daudi Kabaka (Kenya), ambapo abiria anamsihi dereva wa basi aongeze spidi ili abiria afike au awahi “date” yake:
Dereva,
Choma gari moto;
Nifike upesi
Nikaone mtoto.
Mtoto ananingoja
Stendi ya basi;
Fanya haraka!
Kuna pia baadhi ya abiria wenye kutaka kufika mapema kungali na jua kule waendapo. Abiria kama hao huimiza dereva aendeshe kwa kasi.
Madereva wengine nao wanapenda sana kuendesha kwa kasi ili wapate muda wa kupumzika, na kupata angalau “moja baridi” au kuwaona wapenzi wao huko waendapo au mwisho wa safari.
Madereva wengine ni walevi; hupenda kunywa vileo kabla ya safari na wakati mwingine kupumzika safarini kwenye visima vya ulevi.
Ukiwa Dar es Salaam, mabasi ya kwenda katika mikoa mingine yanaitwa “mabasi ya kwenda mikoani”, kana kwamba Dar es Salaam si mkoa.
Kuna mabasi mengine, kwa mfano, huondoka Dar kwenda Mwanza kupitia Nairobi (Kenya) huwa yana madereva wawili tu. Kuna pia mabasi yanayoondoka Dar es Salaam kwenda Lubumbashi huko Kongo (Kinshasa) kupitia Kitwe (Zambia).
Habari za kuaminika zinaeleza kuwa wakati mwingi madereva huchoka kuendesha na kuanza kusinzia sinzia na huku wakiendesha.
Kuna madereva wengine wenye ka-tabia ka kuendesha magari kana kwamba wana-“enjoy the cruising moment.”
Madereva wengine vichwamaji huwazuia wenzao wasipite; ni kama umewatukana. Hivyo huendesha kwa ujeuri kana kwamba kuna ugomvi au vita.
Madereva wengine, hasa kwenye barabara zetu zisizo na lami, wanapenda sana kutangulia kuepuka au kuogopa mavumbi yanayoachwa na gari liliotangulia. Huwa ni mashindano.
Kuna wengine, hasa wamiliki, hupenda sana kushindana kuwa wa kwanza kuchukua abiria au shehena kabla ya wenzao. Tabia hii ni ya kawaida kwenye barabara zetu nyingi.
Dereva wa basi ataliendesha basi lake kwa “ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya” ili awahi kuchuma. Na mara nyingine basi linaweza kupata ajali.
Barabara nyingi hazina maafisa wa trafiki. Na kama wapo wengi wanahongwa; na wananyamaza, kana kwamba mambo yote ni sawia. Lakini ukificha maradhi, kifo kitakuumbua.
Wamiliki wa magari na madereva wamewaweka wakuu wa trafiki wa wilaya na mikoa mikononi. Hata kama afisa wa trafiki mdogo akimkamata mhalifu, kesi yake itafutwa na “wakubwa”.
Barabara: Ripoti hiyo hiyo inaelezea kuwa ajali asili mia 7 husababishwa na matatizo ya barabara.
Napenda kuongezea kuwa barabara zetu ndo hivyo tena; zilitengenezwa wakati magari yalikuwa ni ya serikali au machache kwa ajili ya abiria.
Ieleweke wazi kuwa hakuna uwiano wa moja kwa moja kati ya barabara nzuri na kupungua kwa ajali.
Huko Ulaya kufika mwaka 1648, barabara zake nyingi zilizokitengenezwa tangu enzi za Warumi zilikarabatiwa kukabili mapinduzi ya viwandani yaliyoleta magari ya kukokotwa na farasi hadi mwingilio wa magari ya sasa.
Huko Ulaya, Ujerumani wakati wa Hitler ikawa ya kwanza kuwa na “autobahns” “highways”) kukidhi mahitaji wa maendeleo ya uchumi wa nchi hiyo na endapo kutatokea vita.
Nchi nyingi za Ulaya/Amerika na zingine zilizoendelea zina barabara nzuri na pana. Nitatoa mfano mdogo wa hapa Amerika:
New Jersey Turnpike (Highway) ipitayo karibu na Newark Liberty International Airport ina barabara zenye safu (lanes) sita za kwenda upande mmoja. Kwahiyo barabara kuu hiyo ni kama ina barabara 12. “Highways” nyingi zina safu 3.
Kwa kuwa Amerika inaendeshea mkono wa kushoto, safu ya upande wa kushoto ni kwa wale wenye kutaka kwenda kasi bila ku- “exit”. Safu ya katikati ni kwa wale wenye kuendesha mwendo wa kawaida. Na safu ya upande wa kulia ni kwa wale wenye kutaka ku-“exit”.
Pamoja na “administration and management” ya uedeshaji wa namna hiyo, kuna matrafiki wakali wa mikoa (State Troopers) wanaolinda sheria za barabarani. Wengine hufanya kazi zao wazi wazi.
Endapo msafara wa magari unakwenda kwa kasi, gari la trafiki hao litatangulia mbele na kwenda spidi inayotakiwa. Hakuna dereva atakayethubutu kuli-“overtake”!
Kuna wakati madereva iliwabidi kuwasiliana kwa njia ya "Citizen Band - CB" ili kujiepusha na "State Troopers".
Wakati mwingine matrafiki hao hujificha vichakani kando ya marabara na kuwalopoa (kwa njia ya rada) wale wenye ku-“overspeed”, na wakati mwingine kufanya ukaguzi wa ghafula wa gari.
Magari ya kubeba shehena (“rigs” au “long distance trucking or haulage”) haya yana sheria zake kali. Kila dereva ni lazima abebe utambulisho wa kile alichobeba, kinatoka na kwenda wapi, ameanza kuendesha saa ngapi, na amepumzika kwa kiasi gani. Gari lake pia ni lazima lionyeshe ukaguzi uliofanyika.
Na katika mabarabara ya mikoa mingi kuna “weighing stations” za kupima magari hayo yamebeba shehena ya uzito gani, pamoja na kuchunguza mambo mengine muhimu ya ki-trafiki.
Dereva mwenye hatia, hutozwa faini pamoja na kupoteza pointi fulani kutoka kwa leseni yake, hadi kiasi cha kutoruhusiwa kuendesha.
Gari: Ripoti hiyo niliyotaja hapo juu inaeleza kwa ajali asili mia 1 husababishwa na gari lenyewe.
Napenda kuongezea kuwa baadhi yetu wanaweza kusema gari haliui; anayeua ni dereva, sawa na kusema kuwa bunduki haiui; anayeua ni mwanadamu.
Gari halina budi kuwa katika hali nzuri ya kuendeshwa. Matairi yawe katika hali nzuri na kiasi cha upepo uliojazwa, na viungo vingine muhimu vya gari vichunguzwe mara kwa mara kuona na kuhakikisha kuwa havina kasoro. Gari ni lazima lifanyiwe “servicing”.
Kuna ka-tabia ka kupenda kutunza pesa kwa madai kwamba gari bado linakwenda. Wamiliki hawapendelei kukarabati magari yao.
Ajali nyingi zinazotokea huwa ni za mabasi mapya. Hii haina maana kuwa basi jipya halipati ajali.
Mengine huanguka kwa sababu ya spidi (ku-“overtake”) na kujaza abiria na shehena (overload).
Mara nyingi mabasi ya namna hiyo hushindwa ku-“balance” kutokana na mshituko wa kona au kwa ghafla kujaribu kukwepa wakati wa ku-“overtake”.
Nchini Amerika ni Jimbo la Connecticut peke yake lenye 55 m.k.s. (majimbo mengi yanaendesha 60, 65, 70 na 75 m.k.s.). Lakini takwimu za spidi na ajali hazikubaliani. Hakuna uwiano kati ya spidi kali na kutokea kwa ajali!
Pengine hii ni kwa sababu ya huduma za haraka za ambulance na hospitali katika kunusuru waliojeruhiwa. Kukosekana kwa huduma za namna hiyo nchini Tanzania kunawafanya waliojeruhiwa kutokwa damu sana. Lakini hapa Amerika endapo itatokea ajali, basi magari huwa yanavaana nyuma kwa nyuma.
Kumekuwepo na ajali nyingi za mashangigi nchini mwetu. Lakini hatuna utafiti yakini wa kuonyesha au kuelezea ni mashangigi ya aina gani au modeli gani, ua magurudumu ya aina gain hupasuka pasuka na kusababaisha ajali.
Wakati mwingine, gari au matairi yake huwa vina hitilafu ambazo madereva wengi hawazifahamu!
Ajali nyingine hapa Amerika zimesababishwa na hililafu, kama nilivyoelezea hapo juu. Ikibainika kuwa aina au modeli fulani ya magari au matairi ndio yenye makosa, basi aina au modeli au matairi hayo yatarejeshwa viwandani.
Je, Tanzania itahakikishaje kuwa hitilafu kama hizo, na makosa mengineyo yanadhibitiwa?
Yasemekana Tanzania yetu ni maskini haiwezi kutengeneza barabara kama za Ulaya/Amerika au kuwa na teknolojia ya kisasa ya kudhibiti nidhamu ya uendeshaji na upakizi.
Nakubalina na hilo hapo juu.
Lakini kuna mengi ya kufanya kudhibiti ajali barabarani.
Mabasi kutoka na kurudi Mwanza/Dar yanayopitia nchi ya jirani ingefaa yawe na madereva wanne. Mmoja kati ya Dar na Arusha (apumzikie Arusha); Arusha na Nairobi (apumzikie Nbi); Nairobi na Tarime (apumzikie Tarime); na Tarime na Mwanza (apumzikie Mwanza). Kila dereva aweze kuendesha kwa muda wa kati ya masaa manane na masaa kumi hivi.
Mabasi yanayokwenda Lubumbashi (Kongo-Kinshasa) nayo yadhibitiwe kikamilifu: Dar hadi Iringa; Iringa hadi Tunduma; Tunduma hadi Kitwe. Kitwe hadi Lubumbashi.
Kuhusu madereva, sioni sababu kwa nini kusiwe na matrafiki wa tarafa au wilaya. Hawa matrafiki wetu waheshimike na wapokezane zamu toka tarafa hadi tarafa au toka wilaya hadi wilaya.
Na kama madereva watathubutu kuwahonga, watahonga mpaka lini? CID, TAKUKURU. na Usalama wa Taifa viwashughulikie!
Yafaa sana mabasi yawekewe ratiba na yazifuate ili kuzuia hiyo “marathon” ya uchu wa kuchuma pesa.
Tuwape madereva mafunzo bora ya usanii elekevu wao kupitia semina, majopo au mikutano sawa na “refresher courses” za kuzidi kunoa umahiri wa kuendesha.
Pengine haitawezekana kuwakutanisha maderera wetu huko Ngurdoto Hotel au Bagamoyo!
Lakini tunaweza kupitia kwenye restauranti za “Mama Ntilie” ili nao wapate mtaji wa kuendeleza ulishaji mijini kwa walalahoi.
Kwa wale madereva wanaoendesha wakubwa, mara nyingi kumekuwepo na malalmiko ya hao madereva kutopata muda wa kupumzika wawapo safarini.
Badala ya kumwambia dereva aende akapumzike na aje amchukue wakati fulani, dereva huyo analazimika kungojea kwenye gari bosi wake amalize shughuli rasmi au za ubinafsi hadi zaidi ya usiku wa manane! Dereva anaambiwa kuanza safari ndefu asubuhi na mapema, tuseme kurudi Dar es Salaam. Na wakati mwingine madereva hao hata posho hawapati vizuri!
Tatizo la kupakia abiria na shehena nyinginezo zaidi ya kilichoruhusiwa, limesababaisha ajali kwa vyombo vetu vya usafiri si barabarani tu bali pia relini, angani na majini.
Gari la moshi lilishindwa kupanda miinuko na ghafla ku-“reverse” na kurudililipotoka. Ndege zetu nyingine zimeshindwa kuruka shauri ya uzito wa shehena (magunia ya vyakula na matunda). Meli, boti, mashua na mitumbwi yetu imezama shauri ya uchu wa pesa kutokana kujaza sana abiria na shehena.
Umuhimi wa “servicing” uzingatiwe na kuelezeka kwa msemo wa mambo ya uganga, “Wakia moja ya kinga ni bora kuliko tani ya tiba.”
Tanzania si masikini; ni tajiri. Tunafuja mapesa yetu bure. Fikiria, hao mawaziri karibu sitini ya 60 ni wa nini, kama sio kuzidi kutonesha kidonda cha umasikini wetu? Hawa “mawaziri” na “wizara” zao wanamaliza mapesa kwa mishahara ya wafanyakazi, kuwapamba kwa magari ya fahari na majumba, marupurupu, ubadhirifu, ufisadi, na kurudufisha huduma.
Tulishindana na Benki Kuu ya Dunia, washauri wetu wa uchumi, kututaka tupunguze sekta ya umma (serikali) ambayo ilikuwa imetuna, mithili ya mwenye kitambi.
Tukashauriwa kuipeleka “gym” ikafanye mazoezi ya kukonda; ikakonda! Lakini sasa tumerudia yale yale ya kuota kitambi, tena kikubwa zaidi! Ikiwa kitambi kwa binadamu leo hii ni “skandali”, basi hata kitambi cha serikali nacho ni “skandali”!
Najua nchi kongwe (kama Uingereza, Ujerumani, Ufaransa) zilikuwa tayari na dola (the State) kabla vyama vya siasa kuanzishwa. Nchi changa (kama Tanzania) zilikuwa ni lazima ziunde vyama vya siasa ili zijenge (the State) na State ijenga nchi. Kwa kifupi, chama tawala cha siasa ndicho kiliunda State ijenga nchi. Matokeo ya kuota kitambi kitambi hicho yalikuwa ni mafanikio ya kujenga nchi.
Leo hii eti tunaambiwa mambo yamebadilika. Kuna kuoana baina ya sekta ya ummana ya binafsi. Ndoa hiyo ndio kitovu cha maendeleo ya kujenga nchi….bado tunajenga nchi mpaka leo! Ubinafsi tuliouona kwa darubini ya ujamaa kuwa kama dhambi, leo hii ni nyenzo muhimu ya kuleta eti maendeleo!
Tunalipendelea sana Jiji la Dar es Salaam. Wengine kati yetu wanalifananisha na New York au Shanghai kwa madhari yake. Tuliache Jiji hili lilivyo bila ya kulinyonga.
Lakini Jiji la Dar limeshindwa kudhibiti wingi wa magari kwenye barabara zilizotengenezwa wakati wa Gavana akiwa ndiye mwenye gari, na wakati wa kutaka kutoka na gari hilo, barabara zilifungwa.
Mpaka sasa, serikali imekataa kuhamia Dodoma; inazidi kujenga nyumba za mawaziri mjini hapo Dar! Nchi imetumia mapesa mengi kwa ajili ya hayo “makao Makuu ya Dodoma” toka enzi za “Sir” George Clement Kahama! Na “over cost” yake inazidi kila mwaka,licha ya kutojua ni mapesa mangapi Mamlaka ya Mji wa Dodoma ilitumia kuwakopesha wafanyakazi wake kujijengea nyumba zao binafsi! Tuache kuhamia Dodoma! TAKUKURU mnayajua hayo!
Itatubidi tuunde utaratibu wetu wenyewe wa madaraka mikoani ili kuendeleza baadhi ya miji yetu mingine na kupunguza msongamano wa magari jijini Dar,ikiwa ni pamoja na watu kusafiri kwendaDar es Salaam kwa ajili ya kununua vitu na huduma.
Niruhusu nifupishe orodha ya wizara zetu ziwe wizara 15 tu. Orodha iwe fupi kama mini-sketi lakini ndefu kiasi cha kusetri huduma za lazima, kama ifuatavyo:
Dar es Salaam: Fedha na Menejimenti ya Utumishi wa Umma; Mipango (Mipango, Uchumi, Uwezeshaji na Kazi); Habari, Utamaduni na Michezo; Nje (Mambo ya Nje, Mashirika ya Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Mashariki); na Ulinzi na JKT.
Dodoma: Uhusiano wa Ndani (Muungano, Siasa na Uhusiano wa Bunge); Elimu (Elimu, Ufundi, Sayansi na Teknolojia; Sheria (Katiba na Utawala Bora); pamoja na kuwa Makao Makuu ya Vyama vya Siasa.
Arusha: Maendeleo (Makazi, Jamii, Jinsia na Watoto); Mambo ya Ndani na Usalama wa Raia; ikiwa ni pamoja na kutoa huduma kwa Nairobi na Kenya Kusini.
Mwanza: Afya na Ustawi wa Jamii, na Mazingira Nishati, Madini na Miundombinu, ikiwa ni pamoja na kuwa jiji la kuhudumia biashara ya Ziwa Victoria, Uganda, na sehemu za Kenya Magharibi.
Kigoma: Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa na Maendeleo ya Vijana, ikiwa ni pamoja na kutoa huduma kwa biashara ya Ziwa Tanganyika, na DCR Mashariki.
Mtwara: Uzalishaji (Viwanda, Biashara na Masoko). Mtwara hauna budi kupewa hadhi mpya kama mji wa huduma za mpango wa “Mtwara Corridor” (Tanzania, Malawi na Zambia na sehemu za Msumbiji Kasikazini). “Daraja la Umoja” kwenye Mto Ruvuma ili kuunganisha Tanzania na Msumbiji sasa linajengwa baada ya kulisubiri kwa miaka mingi tangu Awamu ya Kwanza – wakati Msumbiji inapata uhuru wake!
Mbeya: Ardhi, Maji, Mifugo, Kilimo, Chakula na Ushirika; ikiwa ni pamoja na kutoa huduma kwa nchi za Malawi na Zambia. Ni kitu cha kutia shime kuona kuwa uwamja wa ndege wa kimataifa unaendelea kujengwa mjini Mbeya. Uwanja huu utasaidia pia kuinua maendeleo kwa mikoa ya kusini.
Tuwe na Mawaziri Wadogo 15 tu wakisaidiwa na nyongeza ya Makatibu Wakuu, endapo italazimika. Wizara hizi zitagawanya katika mafungu matano.
Kila fungu litasimamiwa na afisa mwenye sifa za nidhamu na uchapaji kazi ili kuweza kufuatililia maazimio na miradi mbali mbali ya serikali kulingana na”manifesto” ya “chama tawala” (na kudhibitiwa na “chama tawala kivuli” kikisaidiana na vyama vingine vya siasa.
Afisa huyo asaidiane na tawala za mikoa. Wakuu wa mikoa na maafisa wao wasaidizi (hadi wilayani) wafanye kazi karibu zaidi ili kufanikisha wajibu wao kwa wananchi.
Naona kumekuwepo na kuteuliwa kwa maafisa wapya wa kumsaidia Waziri Mkuu katika kusimamia mipango ya sera za serikali.
Hii itasaidia sana kuangalia ni vipi tunavyotekelza yale ya Hotuba Rais aliyotoa alipokifungua Bunge la Awamu ya Nne. Na itawasaidia sana Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kuweza kufuatilia, kukagua na kudhibiti miradi na maazimio yaliyowekwa.
Sambamba na kupunguza wingi wa wizara, juhudi ifanywe pia kupunguza idadi ya wa-Bunge wetu! Wa-Bunge wengine “hulala sana”! Sioni sababu kwa nini kila wilaya isiwe na na m-Bunge mmoja tu wa kuiwakilisha katika Bunge la Taifa, Dodoma!
Shughuli za “wa-Bunge” wa Seriali za Mitaa wapewe hadhi na majukumu makubwa ya kusimamia maendeleo katika sehemu zao za majimbo ya uchaguzi, kulingana ana usemi wa serikali za mitaa wa nchi moja iliyoendelea: “Using local people, with local knowledge to serve the local area”.
Huku tukitilia mkazo wa sera ya “madaraka mikoani” (kama kweli bado inatekelezwa), mikoa yetu haina budi kushiriki zaidi katika kupanga na kutekeleza hayo ya “maisha bora kwa kila m-Tanzania”, ikiwa ni pamoja na kudhibiti athari za ajali barabarani.
Naamini Tanzania si masikini; ni tajiri! Fikiria leo hii tunajivuna kuwa tu nchi ya tatu katika Bara la Afrika kwa uzalishaji wa dhahabu!
Michanga ya dhahabu inachimbwa na kusafirishwa nchi za nje. Makapuni ya kigeni kwa muda wa miaka mitatu ya kuvuna dhahabu yetu bila kulipa kodi.
Yanaweza kuichimba usiku na mchana kabla ya miaka hiyo mitatu kuisha. Miaka mitatu iishapo, ili yaanze kulipa kodi, aidha yanaweza kulalamika kuwa yatafunga migodi kutokana na uhaba au ugumu wa kuchimba dhahabu yenyewe.
Au wakati mwingine makampuni hao yanatishiwa na wakubwa wenye kutaka kuila Tanzania kwa kuyalazimisha kuwahonga ili waidhinishe mikataba hiyo na kuanza kulipa kodi. Hii inayafanya makampuni hayo kuuza “business” kwa wamiliki wengine wa kigeni au kuunda kampuni mpya yenye jina tofauti!
Tatizo hili lipo pia katika mikataba ya gesi yetu. Utajiri wa madini na gesi yetu umeingiliwa na unyarubanja unaotekelezwa na wawekezaji wa kigeni Makampuni hayo yamepewa dhahabu ya bure.
Mikataba tunatiliana na hao wawekezaji wageni ikiwa na kipengere cha “production sharing agreement”, psa (kugawana uzalishaji).
Lakini inaonekana kuwa wanaonufaika na kipengere hiki ni wawekezaji, ambao kila mra huongeza vikampuni vingine vya kigeni vidogo vidogo na kunufaika.
Je, huo si “unyarubanja”?
Hakuna hata kikampuni cha wazawa kinachonufaika na kipengere hicho, kama ilivyo katika mikataba ya madini na gesi yetu. Labda, Tanzania iko pembeni mwa kipengere hicho!
Tangu mkataba wa kwanza kusainiwa (na pengine mpaka sasa hivi) kuna kutafuta “production sharing agreement”, psa (kugawana uzalishaji). Si ajabu mzozo wa Buzwangi umetokana na “production sharing agreement”, kama ilivyo mikataba mingi ya madini na gesi yetu!
Ukifungua http://www.globeinvestor.com/servlet/story/RTGAM.20071030.wbarrick1030/GIStory/ utapata ripoti ya mgomo unaoendelea huko kwenye Mgodi wa Barrick. Mwisho wa stori hii kuna para moja juu ya vile walivyovuna mwaka uliopita:
“The mine, which Barrick acquired in 1999, produced 330,000 ounces of gold last year at a total cash cost of $339 (U.S.) an ounce. It had proven and probable reserves of 11.2 million ounces as of the end of last year.”
Sijui kama wameanza kulipa kodi au kutupatia 3% (royalities) zetu? Hata kama wakitupa kiasi hicho, Tanzania itapata dola ngapi? Fanya hesabu!
Mwisho, naipongeza serikali kwa juhudi zake za kuwapa msasa kidogo madereva. Lakini hii haitoshi kabisa. Naomba juhudi hii isiwe ndani ya majengo tu bali huko nje barabarani ambako ajali hutokea.
Matrafiki wafanye hiyo kwa maadili ya hali ya juu (mithili ya madaktari na wahubiri dini) ili kuokoa maisha na mali ya wa-Tanzania.
Hivi karibuni tulizawadishwa na serikali ya Amerika (kupitia mfuko wa Rais wa Millennium Challenge Corporation - MCC) ya zawadi (“grant”) ya dola 698 milioni kuboresha mabarabara nishati na maji nchini kwa kipindi cha miaka mitano.
Pili, kulikuwa na habari kutoka Makao Makuu ya African Development Bank mjini Tunis kuwa Benki hiyo imetoa kiasi cha dola za ki-Marekani million 92 (72%) (serikali ya Tanzania itagharimia 28%) kwa ajili ya kutengeneza mabarabara ya mikoa ya Dodoma na Singida ili kuuunganisha mikoa na mikoa ya kasikazini hadi Kenya.
Je, ki-mapatano, mapesa hayo yatatumikaje katika kudhibiti baadhi ya mienendo mibaya yetu inayosababisha ajali barabarani?
Hivi karibuni, katika mojawapo ya blogu nyingi mashuhuri za wa-Tanzania, niliahidi kwa kuwaomba wanakijiji kujipa muda wa tutafakuri na kuchangia suala la ajali barabarani na jinsi ambavyo tunaweza kupunguza “balaa” hili ambalo linaendelea kutusibu siku hadi siku, mchana na usiku.
Ingawa ni wanakijiji kama wawili hivi walichangia, sikukata tamaa.
Nazidi kuwaombeni tujaze blogu hizi kwa maoni yetu kuhusu maafa ya ajali barabarani. Blogu hizi zinasomwa na wengi, wakiwemo viongozi wa serikali, wabunge wetu, viongozi wa dini na mashirika yasiyo ya serikali.
Napenda kurudia mchango wangu wa awali kuhusu ajali nchini mwetu, ikiwa ni sehemu ya maombolezo ya kutokwa na Naibu Waziri Salome Mbatia. Mhariri wa gazeti maarufu nchini la kila siku aliandika, “…taifa limeghubikwa na majonzi makubwa kufuatia kifo (cha Naibu Waziri Salome Mbatia) kilichotokana na ajali ya gari eneo la Kibena, Njombe mkoani Iringa Alhamisi.”
Lakini yatubidi kuzingatia kwamba si Salome Mbatia peke yake aliyekufa katika ajali hiyo. Dereva wake na utingo wa lori nao walikufa.
Na sio ajali hiyo tu iliyotokea siku hiyo na kusababisha mauaji! Karibu watu kama kumi hivi walikufa kwa ajali barabarani siku hiyo! Lakini kifo cha Naibu Waziri Salome Mbatia kimepewa kipaumbele zaidi ya vifo vya wengine. Sababu zinaeleweka; sina haja ya kuzirudia.
Mhariri huyo alitoa tahadhari kali kuitaka “Serikali na vyombo husika na sekta ya usafirishaji” kudhibiti ajali: “[Y]afaa tatizo hili la ajali za barabarani zinazotokana na uzebe na mwendo wa kasi litizamwe tena kwa makini.
Bado linapoteza maisha ya watu wengi wasio na hatia wakati zinaweza kuepukwa. Madereva wengi bado wamekuwa ni vichwa maji katika uendeshaji wao barabarani.”
Kauli kama hiyo ya mhariri, sambamba na kauli nyingi za umma zisizotangazwa, inaitaka serikali yetu kamwe isingoje “kifo cha mzaliwa wa kwanza”, kama mtawala Firauni wa Misri, ndipo iamke na kufanya lolote dhidi ya “janga” hili ambalo hudonoa maisha ya wa-Tanzania wetu!
Tumezoea kusema, “Ajali haina kinga!” Lakini ukweli ni kwamba ajali inaweza ikakingika!
Wengine husema, “Ngoja ajali ziwamalize kwa kumwonea Kabwe Zubeir Zitto!”
Hili nitalizungumzia kwa kifupi:
Katika magazeti na blogu nyingi kumeibuka tabaka la washirikina au niwaite “wanajimu wabaya, watabiri mabaya, wenye ndoto mbaya, wenye maono” wenye kungojea “kiyama” kiikumbe serikali na CCM yake.
Wenzetu wanamwomba m-Bunge wetu “kijana” Zitto Zubeir Kabwe aombe miungu ya huko kwao Kigoma kuweka breki ili isiwamalize wote wale waliomnyoshea kidole - mizimu ya Kigoma inalipa kisasi!
Wanaoanisha msululu wa ajali ambazo zimetokea kwa baadhi ya viongozi wa CCM kufuatia mzozo wa m-Bunge wetu “kijana” Zitto Zubeir Kabwe eti zinatokana na “kumwonea Zitto”!
Natarajia kuchangia hili la mzozo wa Zitto, kulingana na maoni ya wasomi wetu wawili: Prof. Gidion Shoo (Zitto Hakuwatendea Mema Wananchi,” kwa mujibu wa “Kanuni za Bunge”. Msomi mwingine ni Prof. Shivji (Zitto Kabwe’s Suspension an Episode or an Epitah?)
Kero ya Zitto yaonyesha jinsi ambavyo nchi yetu imejigawa. Kuna ukweli kwamba wote hatuimbi, “Tanzania, Tanzania, nakupenda kwa moyo wote; nilalapo nakuota, jina lako ni tamu sana”!
Ni lazima kuna sababu zake, mbali ya vitendo vya rushwa na ufisadi!
Kuna baadhi yetu ambao wamegeuka washirikina na kuonyesha hali ya chini kabisa. Hawa wanaomba mabaya zaidi yawapate wana-CCM, kwa jumla, na hasa wale viongozi waliojeruhiwa katika ajali mbali mbali!
Sioni kama hili ni ombi la kiungwana! Ni matakwa ya wendawazimu kwani endapo CCM inafanya mabaya, kuitakia mabaya nako ni vibaya! Makosa mawili hayajengi au hayazai haki!
Kumtakia mwenzako kifo ni sawa na kumwua tu. Leo tunatakiana vifo; kesho tutauana kimacho macho!
Kuna wengine wenye kuamini kuwa ajali “Ni mipango ya Mungu - Mungu kapenda; siku yako ya kufa ikifika, imefika!”
Hili pia yanataka ufafanuzi:
Je, maisha yetu yamewekewa
“blinkers” za “determinism”? Je, hakuna lolote tunaloweza kufanya kuepusha hiyo “determinism”? Mbona tunataka kuingilia kati nguvu za asili (nature) kwa kualika nchini “wachawi wa mvua” kutoka Thailand?
Maisha yanajengeka kutokana na kuoana kwa akili zetu na maingilio ya mazingira tuliyomo. Tunaweza kuyabadili kwa kupata elimu tosheleza na hekima ya kuweza kutafukari na kutafuta njia za kusuluhisha au kutanzua tatizo la ajali barabarani.
Wengine, hasa wadini walokoke huamini kuwa Mungu huadhibu kwa sababu ya dhambi. Hii sio kwa wa-Tanzania tu bali pia wahubiri wengi walokoke duniani, hususani, Marekani.
Mhubiri mmoja mlokoke wa Amerika aliwahi kutamka kuwa Jimbo la Florida lilipatwa na madhara ya kuwaka moto kutokana na dhambi za kisenge na kishoga.
Mlokoke huyo huyo alimshutumu Waziri Mkuu wa Israel kwa kupatwa na mshituko uliomlemaza kuwa ni kwa sababu kagawa nchi ya Palestine - nchi ya Mungu - kwa Wapalestina!
Kisa kingine cha hivi karibuni: Jaji wa “federal” hapa Amerika ameamuru kanisa moja la Ki-Baptist la Westboro - kanisa lenye kuhubiri na kueneza chuki - kulipa faini ya dola millioni 10.9 kwa kushangilia kifo na kukielezea kifo hicho cha askari Lance Cpl Matthew Snyder vitani Iraq Machi 2006 kuwa ni adhabu kutoka kwa Mungu.
Washirika walokoke wengi wa hapa Amerika wanahubiri ‘injili ya chuki” dhidi ya ushoga na kubagua mazishi ya watu waliokufa kwa ukimwi. Walokole wengine wanaamini kuwa Amerika inapata majanga, kama hilo la 911, kwa sababu wameacha kumcha Mungu!
Je, Mungu anatuadhibu na hizo ajali zitokeazo barabarani?
Pengine hilo la ajali na kudra za Mwenyenzi Mungu nalo linahitaji muda wake maalum wa kutafukari kwa undani, hasa kwa wale wenye kutaka kujua kutoka kwa wanaolielewa vizuri.
Kuna baadhi yetu wenye kuziona na kuzitafukari ajali barabarani na kwinginepo, kama matukio ya kawaida tu. Tusitekwe nyara na fikra za kufungwa macho yetu na akili zetu kuamini kwamba ajali haina kinga; ajali ni adhabu ya Mungu, au ni matakwa mengine ya ushirikina. Ajali husababishwa na/au mchanganyiko wa haya matatu:
dereva, gari na barabara.
Kuna Ripoti ya Mwaka 1994 inayoelezea rasmi na kwa undani kuhusu usafiri nchini. Sijui ni wangapi kati ya matrafiki husika, wamiliki wa magari, maderera na abiria wa kawaida wameipitia ripoti hii?
Kuna vitu vitatu muhimu katika njia za usafiri wa nchi kavu kwa kutumia magari barabarani: dereva, gari na barabara. Kila kimoja kina masharti yake sawa na “social environment”: mshiriki (actor/participant), kusudi (purpose), sheria (rules and regulations), mipaka (boundaries), maadili (morality), siasa (what is to be done), na lugha (technical language).
Dereva: Kulingana na Ripoti hiyo, sababu kubwa ya ajali nchini mwetu hutokana na madreva wenyewe. Ajali za namna hii ni kiasi cha asilimia 76.
Napenda kuongezea kuwa u-mahiri na u-makini wa kuendesha unatokana na mafunzo tosheleza na utahini usiopendelea; dereva kujiandaa vya kutosha kabla ya safari; asiendeshe huku amelewa au amechoka; afuate sheria za barabarani; na uwezo wa dereva kubaini endapo gari lake lina udhaifu au kasoro.
Ajali nyingi za mabasi, malori yetu na magari madogo yetu kugongana vichwa kwa vichwa, kama ajali hiyo iliyotokea na na kuchukua maisha ya wakina Waziri Mbatia, dereva na utingo wa lori.
Hii ina maana kuwa sababu kubwa ni pale dereva wa gari linalofuata kutaka ku-“overtake” lililotangulia karibu na mwisho wa kilima au kwenye kona kali bila kujua kuwa kuna gari lingine linakuja mbele.
Wakati mwingine gari hupata kasoro na dereva kushindwa kuliongoza. Sababu nyingine ni kwa dereva kuchoka na kusinzia sinzia na mwisho kupoteza saiti yake.
Madereva wengine huendesha kulingana na wimbo wa mapenzi wa Daudi Kabaka (Kenya), ambapo abiria anamsihi dereva wa basi aongeze spidi ili abiria afike au awahi “date” yake:
Dereva,
Choma gari moto;
Nifike upesi
Nikaone mtoto.
Mtoto ananingoja
Stendi ya basi;
Fanya haraka!
Kuna pia baadhi ya abiria wenye kutaka kufika mapema kungali na jua kule waendapo. Abiria kama hao huimiza dereva aendeshe kwa kasi.
Madereva wengine nao wanapenda sana kuendesha kwa kasi ili wapate muda wa kupumzika, na kupata angalau “moja baridi” au kuwaona wapenzi wao huko waendapo au mwisho wa safari.
Madereva wengine ni walevi; hupenda kunywa vileo kabla ya safari na wakati mwingine kupumzika safarini kwenye visima vya ulevi.
Ukiwa Dar es Salaam, mabasi ya kwenda katika mikoa mingine yanaitwa “mabasi ya kwenda mikoani”, kana kwamba Dar es Salaam si mkoa.
Kuna mabasi mengine, kwa mfano, huondoka Dar kwenda Mwanza kupitia Nairobi (Kenya) huwa yana madereva wawili tu. Kuna pia mabasi yanayoondoka Dar es Salaam kwenda Lubumbashi huko Kongo (Kinshasa) kupitia Kitwe (Zambia).
Habari za kuaminika zinaeleza kuwa wakati mwingi madereva huchoka kuendesha na kuanza kusinzia sinzia na huku wakiendesha.
Kuna madereva wengine wenye ka-tabia ka kuendesha magari kana kwamba wana-“enjoy the cruising moment.”
Madereva wengine vichwamaji huwazuia wenzao wasipite; ni kama umewatukana. Hivyo huendesha kwa ujeuri kana kwamba kuna ugomvi au vita.
Madereva wengine, hasa kwenye barabara zetu zisizo na lami, wanapenda sana kutangulia kuepuka au kuogopa mavumbi yanayoachwa na gari liliotangulia. Huwa ni mashindano.
Kuna wengine, hasa wamiliki, hupenda sana kushindana kuwa wa kwanza kuchukua abiria au shehena kabla ya wenzao. Tabia hii ni ya kawaida kwenye barabara zetu nyingi.
Dereva wa basi ataliendesha basi lake kwa “ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya” ili awahi kuchuma. Na mara nyingine basi linaweza kupata ajali.
Barabara nyingi hazina maafisa wa trafiki. Na kama wapo wengi wanahongwa; na wananyamaza, kana kwamba mambo yote ni sawia. Lakini ukificha maradhi, kifo kitakuumbua.
Wamiliki wa magari na madereva wamewaweka wakuu wa trafiki wa wilaya na mikoa mikononi. Hata kama afisa wa trafiki mdogo akimkamata mhalifu, kesi yake itafutwa na “wakubwa”.
Barabara: Ripoti hiyo hiyo inaelezea kuwa ajali asili mia 7 husababishwa na matatizo ya barabara.
Napenda kuongezea kuwa barabara zetu ndo hivyo tena; zilitengenezwa wakati magari yalikuwa ni ya serikali au machache kwa ajili ya abiria.
Ieleweke wazi kuwa hakuna uwiano wa moja kwa moja kati ya barabara nzuri na kupungua kwa ajali.
Huko Ulaya kufika mwaka 1648, barabara zake nyingi zilizokitengenezwa tangu enzi za Warumi zilikarabatiwa kukabili mapinduzi ya viwandani yaliyoleta magari ya kukokotwa na farasi hadi mwingilio wa magari ya sasa.
Huko Ulaya, Ujerumani wakati wa Hitler ikawa ya kwanza kuwa na “autobahns” “highways”) kukidhi mahitaji wa maendeleo ya uchumi wa nchi hiyo na endapo kutatokea vita.
Nchi nyingi za Ulaya/Amerika na zingine zilizoendelea zina barabara nzuri na pana. Nitatoa mfano mdogo wa hapa Amerika:
New Jersey Turnpike (Highway) ipitayo karibu na Newark Liberty International Airport ina barabara zenye safu (lanes) sita za kwenda upande mmoja. Kwahiyo barabara kuu hiyo ni kama ina barabara 12. “Highways” nyingi zina safu 3.
Kwa kuwa Amerika inaendeshea mkono wa kushoto, safu ya upande wa kushoto ni kwa wale wenye kutaka kwenda kasi bila ku- “exit”. Safu ya katikati ni kwa wale wenye kuendesha mwendo wa kawaida. Na safu ya upande wa kulia ni kwa wale wenye kutaka ku-“exit”.
Pamoja na “administration and management” ya uedeshaji wa namna hiyo, kuna matrafiki wakali wa mikoa (State Troopers) wanaolinda sheria za barabarani. Wengine hufanya kazi zao wazi wazi.
Endapo msafara wa magari unakwenda kwa kasi, gari la trafiki hao litatangulia mbele na kwenda spidi inayotakiwa. Hakuna dereva atakayethubutu kuli-“overtake”!
Kuna wakati madereva iliwabidi kuwasiliana kwa njia ya "Citizen Band - CB" ili kujiepusha na "State Troopers".
Wakati mwingine matrafiki hao hujificha vichakani kando ya marabara na kuwalopoa (kwa njia ya rada) wale wenye ku-“overspeed”, na wakati mwingine kufanya ukaguzi wa ghafula wa gari.
Magari ya kubeba shehena (“rigs” au “long distance trucking or haulage”) haya yana sheria zake kali. Kila dereva ni lazima abebe utambulisho wa kile alichobeba, kinatoka na kwenda wapi, ameanza kuendesha saa ngapi, na amepumzika kwa kiasi gani. Gari lake pia ni lazima lionyeshe ukaguzi uliofanyika.
Na katika mabarabara ya mikoa mingi kuna “weighing stations” za kupima magari hayo yamebeba shehena ya uzito gani, pamoja na kuchunguza mambo mengine muhimu ya ki-trafiki.
Dereva mwenye hatia, hutozwa faini pamoja na kupoteza pointi fulani kutoka kwa leseni yake, hadi kiasi cha kutoruhusiwa kuendesha.
Gari: Ripoti hiyo niliyotaja hapo juu inaeleza kwa ajali asili mia 1 husababishwa na gari lenyewe.
Napenda kuongezea kuwa baadhi yetu wanaweza kusema gari haliui; anayeua ni dereva, sawa na kusema kuwa bunduki haiui; anayeua ni mwanadamu.
Gari halina budi kuwa katika hali nzuri ya kuendeshwa. Matairi yawe katika hali nzuri na kiasi cha upepo uliojazwa, na viungo vingine muhimu vya gari vichunguzwe mara kwa mara kuona na kuhakikisha kuwa havina kasoro. Gari ni lazima lifanyiwe “servicing”.
Kuna ka-tabia ka kupenda kutunza pesa kwa madai kwamba gari bado linakwenda. Wamiliki hawapendelei kukarabati magari yao.
Ajali nyingi zinazotokea huwa ni za mabasi mapya. Hii haina maana kuwa basi jipya halipati ajali.
Mengine huanguka kwa sababu ya spidi (ku-“overtake”) na kujaza abiria na shehena (overload).
Mara nyingi mabasi ya namna hiyo hushindwa ku-“balance” kutokana na mshituko wa kona au kwa ghafla kujaribu kukwepa wakati wa ku-“overtake”.
Nchini Amerika ni Jimbo la Connecticut peke yake lenye 55 m.k.s. (majimbo mengi yanaendesha 60, 65, 70 na 75 m.k.s.). Lakini takwimu za spidi na ajali hazikubaliani. Hakuna uwiano kati ya spidi kali na kutokea kwa ajali!
Pengine hii ni kwa sababu ya huduma za haraka za ambulance na hospitali katika kunusuru waliojeruhiwa. Kukosekana kwa huduma za namna hiyo nchini Tanzania kunawafanya waliojeruhiwa kutokwa damu sana. Lakini hapa Amerika endapo itatokea ajali, basi magari huwa yanavaana nyuma kwa nyuma.
Kumekuwepo na ajali nyingi za mashangigi nchini mwetu. Lakini hatuna utafiti yakini wa kuonyesha au kuelezea ni mashangigi ya aina gani au modeli gani, ua magurudumu ya aina gain hupasuka pasuka na kusababaisha ajali.
Wakati mwingine, gari au matairi yake huwa vina hitilafu ambazo madereva wengi hawazifahamu!
Ajali nyingine hapa Amerika zimesababishwa na hililafu, kama nilivyoelezea hapo juu. Ikibainika kuwa aina au modeli fulani ya magari au matairi ndio yenye makosa, basi aina au modeli au matairi hayo yatarejeshwa viwandani.
Je, Tanzania itahakikishaje kuwa hitilafu kama hizo, na makosa mengineyo yanadhibitiwa?
Yasemekana Tanzania yetu ni maskini haiwezi kutengeneza barabara kama za Ulaya/Amerika au kuwa na teknolojia ya kisasa ya kudhibiti nidhamu ya uendeshaji na upakizi.
Nakubalina na hilo hapo juu.
Lakini kuna mengi ya kufanya kudhibiti ajali barabarani.
Mabasi kutoka na kurudi Mwanza/Dar yanayopitia nchi ya jirani ingefaa yawe na madereva wanne. Mmoja kati ya Dar na Arusha (apumzikie Arusha); Arusha na Nairobi (apumzikie Nbi); Nairobi na Tarime (apumzikie Tarime); na Tarime na Mwanza (apumzikie Mwanza). Kila dereva aweze kuendesha kwa muda wa kati ya masaa manane na masaa kumi hivi.
Mabasi yanayokwenda Lubumbashi (Kongo-Kinshasa) nayo yadhibitiwe kikamilifu: Dar hadi Iringa; Iringa hadi Tunduma; Tunduma hadi Kitwe. Kitwe hadi Lubumbashi.
Kuhusu madereva, sioni sababu kwa nini kusiwe na matrafiki wa tarafa au wilaya. Hawa matrafiki wetu waheshimike na wapokezane zamu toka tarafa hadi tarafa au toka wilaya hadi wilaya.
Na kama madereva watathubutu kuwahonga, watahonga mpaka lini? CID, TAKUKURU. na Usalama wa Taifa viwashughulikie!
Yafaa sana mabasi yawekewe ratiba na yazifuate ili kuzuia hiyo “marathon” ya uchu wa kuchuma pesa.
Tuwape madereva mafunzo bora ya usanii elekevu wao kupitia semina, majopo au mikutano sawa na “refresher courses” za kuzidi kunoa umahiri wa kuendesha.
Pengine haitawezekana kuwakutanisha maderera wetu huko Ngurdoto Hotel au Bagamoyo!
Lakini tunaweza kupitia kwenye restauranti za “Mama Ntilie” ili nao wapate mtaji wa kuendeleza ulishaji mijini kwa walalahoi.
Kwa wale madereva wanaoendesha wakubwa, mara nyingi kumekuwepo na malalmiko ya hao madereva kutopata muda wa kupumzika wawapo safarini.
Badala ya kumwambia dereva aende akapumzike na aje amchukue wakati fulani, dereva huyo analazimika kungojea kwenye gari bosi wake amalize shughuli rasmi au za ubinafsi hadi zaidi ya usiku wa manane! Dereva anaambiwa kuanza safari ndefu asubuhi na mapema, tuseme kurudi Dar es Salaam. Na wakati mwingine madereva hao hata posho hawapati vizuri!
Tatizo la kupakia abiria na shehena nyinginezo zaidi ya kilichoruhusiwa, limesababaisha ajali kwa vyombo vetu vya usafiri si barabarani tu bali pia relini, angani na majini.
Gari la moshi lilishindwa kupanda miinuko na ghafla ku-“reverse” na kurudililipotoka. Ndege zetu nyingine zimeshindwa kuruka shauri ya uzito wa shehena (magunia ya vyakula na matunda). Meli, boti, mashua na mitumbwi yetu imezama shauri ya uchu wa pesa kutokana kujaza sana abiria na shehena.
Umuhimi wa “servicing” uzingatiwe na kuelezeka kwa msemo wa mambo ya uganga, “Wakia moja ya kinga ni bora kuliko tani ya tiba.”
Tanzania si masikini; ni tajiri. Tunafuja mapesa yetu bure. Fikiria, hao mawaziri karibu sitini ya 60 ni wa nini, kama sio kuzidi kutonesha kidonda cha umasikini wetu? Hawa “mawaziri” na “wizara” zao wanamaliza mapesa kwa mishahara ya wafanyakazi, kuwapamba kwa magari ya fahari na majumba, marupurupu, ubadhirifu, ufisadi, na kurudufisha huduma.
Tulishindana na Benki Kuu ya Dunia, washauri wetu wa uchumi, kututaka tupunguze sekta ya umma (serikali) ambayo ilikuwa imetuna, mithili ya mwenye kitambi.
Tukashauriwa kuipeleka “gym” ikafanye mazoezi ya kukonda; ikakonda! Lakini sasa tumerudia yale yale ya kuota kitambi, tena kikubwa zaidi! Ikiwa kitambi kwa binadamu leo hii ni “skandali”, basi hata kitambi cha serikali nacho ni “skandali”!
Najua nchi kongwe (kama Uingereza, Ujerumani, Ufaransa) zilikuwa tayari na dola (the State) kabla vyama vya siasa kuanzishwa. Nchi changa (kama Tanzania) zilikuwa ni lazima ziunde vyama vya siasa ili zijenge (the State) na State ijenga nchi. Kwa kifupi, chama tawala cha siasa ndicho kiliunda State ijenga nchi. Matokeo ya kuota kitambi kitambi hicho yalikuwa ni mafanikio ya kujenga nchi.
Leo hii eti tunaambiwa mambo yamebadilika. Kuna kuoana baina ya sekta ya ummana ya binafsi. Ndoa hiyo ndio kitovu cha maendeleo ya kujenga nchi….bado tunajenga nchi mpaka leo! Ubinafsi tuliouona kwa darubini ya ujamaa kuwa kama dhambi, leo hii ni nyenzo muhimu ya kuleta eti maendeleo!
Tunalipendelea sana Jiji la Dar es Salaam. Wengine kati yetu wanalifananisha na New York au Shanghai kwa madhari yake. Tuliache Jiji hili lilivyo bila ya kulinyonga.
Lakini Jiji la Dar limeshindwa kudhibiti wingi wa magari kwenye barabara zilizotengenezwa wakati wa Gavana akiwa ndiye mwenye gari, na wakati wa kutaka kutoka na gari hilo, barabara zilifungwa.
Mpaka sasa, serikali imekataa kuhamia Dodoma; inazidi kujenga nyumba za mawaziri mjini hapo Dar! Nchi imetumia mapesa mengi kwa ajili ya hayo “makao Makuu ya Dodoma” toka enzi za “Sir” George Clement Kahama! Na “over cost” yake inazidi kila mwaka,licha ya kutojua ni mapesa mangapi Mamlaka ya Mji wa Dodoma ilitumia kuwakopesha wafanyakazi wake kujijengea nyumba zao binafsi! Tuache kuhamia Dodoma! TAKUKURU mnayajua hayo!
Itatubidi tuunde utaratibu wetu wenyewe wa madaraka mikoani ili kuendeleza baadhi ya miji yetu mingine na kupunguza msongamano wa magari jijini Dar,ikiwa ni pamoja na watu kusafiri kwendaDar es Salaam kwa ajili ya kununua vitu na huduma.
Niruhusu nifupishe orodha ya wizara zetu ziwe wizara 15 tu. Orodha iwe fupi kama mini-sketi lakini ndefu kiasi cha kusetri huduma za lazima, kama ifuatavyo:
Dar es Salaam: Fedha na Menejimenti ya Utumishi wa Umma; Mipango (Mipango, Uchumi, Uwezeshaji na Kazi); Habari, Utamaduni na Michezo; Nje (Mambo ya Nje, Mashirika ya Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Mashariki); na Ulinzi na JKT.
Dodoma: Uhusiano wa Ndani (Muungano, Siasa na Uhusiano wa Bunge); Elimu (Elimu, Ufundi, Sayansi na Teknolojia; Sheria (Katiba na Utawala Bora); pamoja na kuwa Makao Makuu ya Vyama vya Siasa.
Arusha: Maendeleo (Makazi, Jamii, Jinsia na Watoto); Mambo ya Ndani na Usalama wa Raia; ikiwa ni pamoja na kutoa huduma kwa Nairobi na Kenya Kusini.
Mwanza: Afya na Ustawi wa Jamii, na Mazingira Nishati, Madini na Miundombinu, ikiwa ni pamoja na kuwa jiji la kuhudumia biashara ya Ziwa Victoria, Uganda, na sehemu za Kenya Magharibi.
Kigoma: Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa na Maendeleo ya Vijana, ikiwa ni pamoja na kutoa huduma kwa biashara ya Ziwa Tanganyika, na DCR Mashariki.
Mtwara: Uzalishaji (Viwanda, Biashara na Masoko). Mtwara hauna budi kupewa hadhi mpya kama mji wa huduma za mpango wa “Mtwara Corridor” (Tanzania, Malawi na Zambia na sehemu za Msumbiji Kasikazini). “Daraja la Umoja” kwenye Mto Ruvuma ili kuunganisha Tanzania na Msumbiji sasa linajengwa baada ya kulisubiri kwa miaka mingi tangu Awamu ya Kwanza – wakati Msumbiji inapata uhuru wake!
Mbeya: Ardhi, Maji, Mifugo, Kilimo, Chakula na Ushirika; ikiwa ni pamoja na kutoa huduma kwa nchi za Malawi na Zambia. Ni kitu cha kutia shime kuona kuwa uwamja wa ndege wa kimataifa unaendelea kujengwa mjini Mbeya. Uwanja huu utasaidia pia kuinua maendeleo kwa mikoa ya kusini.
Tuwe na Mawaziri Wadogo 15 tu wakisaidiwa na nyongeza ya Makatibu Wakuu, endapo italazimika. Wizara hizi zitagawanya katika mafungu matano.
Kila fungu litasimamiwa na afisa mwenye sifa za nidhamu na uchapaji kazi ili kuweza kufuatililia maazimio na miradi mbali mbali ya serikali kulingana na”manifesto” ya “chama tawala” (na kudhibitiwa na “chama tawala kivuli” kikisaidiana na vyama vingine vya siasa.
Afisa huyo asaidiane na tawala za mikoa. Wakuu wa mikoa na maafisa wao wasaidizi (hadi wilayani) wafanye kazi karibu zaidi ili kufanikisha wajibu wao kwa wananchi.
Naona kumekuwepo na kuteuliwa kwa maafisa wapya wa kumsaidia Waziri Mkuu katika kusimamia mipango ya sera za serikali.
Hii itasaidia sana kuangalia ni vipi tunavyotekelza yale ya Hotuba Rais aliyotoa alipokifungua Bunge la Awamu ya Nne. Na itawasaidia sana Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kuweza kufuatilia, kukagua na kudhibiti miradi na maazimio yaliyowekwa.
Sambamba na kupunguza wingi wa wizara, juhudi ifanywe pia kupunguza idadi ya wa-Bunge wetu! Wa-Bunge wengine “hulala sana”! Sioni sababu kwa nini kila wilaya isiwe na na m-Bunge mmoja tu wa kuiwakilisha katika Bunge la Taifa, Dodoma!
Shughuli za “wa-Bunge” wa Seriali za Mitaa wapewe hadhi na majukumu makubwa ya kusimamia maendeleo katika sehemu zao za majimbo ya uchaguzi, kulingana ana usemi wa serikali za mitaa wa nchi moja iliyoendelea: “Using local people, with local knowledge to serve the local area”.
Huku tukitilia mkazo wa sera ya “madaraka mikoani” (kama kweli bado inatekelezwa), mikoa yetu haina budi kushiriki zaidi katika kupanga na kutekeleza hayo ya “maisha bora kwa kila m-Tanzania”, ikiwa ni pamoja na kudhibiti athari za ajali barabarani.
Naamini Tanzania si masikini; ni tajiri! Fikiria leo hii tunajivuna kuwa tu nchi ya tatu katika Bara la Afrika kwa uzalishaji wa dhahabu!
Michanga ya dhahabu inachimbwa na kusafirishwa nchi za nje. Makapuni ya kigeni kwa muda wa miaka mitatu ya kuvuna dhahabu yetu bila kulipa kodi.
Yanaweza kuichimba usiku na mchana kabla ya miaka hiyo mitatu kuisha. Miaka mitatu iishapo, ili yaanze kulipa kodi, aidha yanaweza kulalamika kuwa yatafunga migodi kutokana na uhaba au ugumu wa kuchimba dhahabu yenyewe.
Au wakati mwingine makampuni hao yanatishiwa na wakubwa wenye kutaka kuila Tanzania kwa kuyalazimisha kuwahonga ili waidhinishe mikataba hiyo na kuanza kulipa kodi. Hii inayafanya makampuni hayo kuuza “business” kwa wamiliki wengine wa kigeni au kuunda kampuni mpya yenye jina tofauti!
Tatizo hili lipo pia katika mikataba ya gesi yetu. Utajiri wa madini na gesi yetu umeingiliwa na unyarubanja unaotekelezwa na wawekezaji wa kigeni Makampuni hayo yamepewa dhahabu ya bure.
Mikataba tunatiliana na hao wawekezaji wageni ikiwa na kipengere cha “production sharing agreement”, psa (kugawana uzalishaji).
Lakini inaonekana kuwa wanaonufaika na kipengere hiki ni wawekezaji, ambao kila mra huongeza vikampuni vingine vya kigeni vidogo vidogo na kunufaika.
Je, huo si “unyarubanja”?
Hakuna hata kikampuni cha wazawa kinachonufaika na kipengere hicho, kama ilivyo katika mikataba ya madini na gesi yetu. Labda, Tanzania iko pembeni mwa kipengere hicho!
Tangu mkataba wa kwanza kusainiwa (na pengine mpaka sasa hivi) kuna kutafuta “production sharing agreement”, psa (kugawana uzalishaji). Si ajabu mzozo wa Buzwangi umetokana na “production sharing agreement”, kama ilivyo mikataba mingi ya madini na gesi yetu!
Ukifungua http://www.globeinvestor.com/servlet/story/RTGAM.20071030.wbarrick1030/GIStory/ utapata ripoti ya mgomo unaoendelea huko kwenye Mgodi wa Barrick. Mwisho wa stori hii kuna para moja juu ya vile walivyovuna mwaka uliopita:
“The mine, which Barrick acquired in 1999, produced 330,000 ounces of gold last year at a total cash cost of $339 (U.S.) an ounce. It had proven and probable reserves of 11.2 million ounces as of the end of last year.”
Sijui kama wameanza kulipa kodi au kutupatia 3% (royalities) zetu? Hata kama wakitupa kiasi hicho, Tanzania itapata dola ngapi? Fanya hesabu!
Mwisho, naipongeza serikali kwa juhudi zake za kuwapa msasa kidogo madereva. Lakini hii haitoshi kabisa. Naomba juhudi hii isiwe ndani ya majengo tu bali huko nje barabarani ambako ajali hutokea.
Matrafiki wafanye hiyo kwa maadili ya hali ya juu (mithili ya madaktari na wahubiri dini) ili kuokoa maisha na mali ya wa-Tanzania.
Hivi karibuni tulizawadishwa na serikali ya Amerika (kupitia mfuko wa Rais wa Millennium Challenge Corporation - MCC) ya zawadi (“grant”) ya dola 698 milioni kuboresha mabarabara nishati na maji nchini kwa kipindi cha miaka mitano.
Pili, kulikuwa na habari kutoka Makao Makuu ya African Development Bank mjini Tunis kuwa Benki hiyo imetoa kiasi cha dola za ki-Marekani million 92 (72%) (serikali ya Tanzania itagharimia 28%) kwa ajili ya kutengeneza mabarabara ya mikoa ya Dodoma na Singida ili kuuunganisha mikoa na mikoa ya kasikazini hadi Kenya.
Je, ki-mapatano, mapesa hayo yatatumikaje katika kudhibiti baadhi ya mienendo mibaya yetu inayosababisha ajali barabarani?
25 October 2007
Naibu waziri wa maendeleo ya jamii jinsia na watoto Amefariki dunia.

Ilikuwa jana jioni majira ya saa kumi na moja na nusu jioni ambapo mama yetu mpendwa waziri Salome Joseph Mbatia alikutwa na mauti akiwa kazini. Watanzania tumeipokea habari hii kwa masikitiko makubwa kwani mara nyingi ajali hizi zimekuwa zikisababishwa na uzembe wa madereva na serikali kutokuwa wakali na makini katika sheria za barabarani. Kwa mara nyingine tena tunaiomba serikali iache kuzembea katika suala hili la matumizi ya barabara. Kwa habari zaidi Soma hapa.

Pichani juu ni ajali yenyewe ilivyokuwa.Mungu amlaze mahali pema Amina.
Picha kwa hisani ya Haki Ngowi
21 October 2007
Sanaa hii ni ya nani?
Unajua mara nyingi mtu au kitu hutambulika kutokana na mtindo wake, Leo nina swali juu ya picha hapo juu, Je sanaa au michoro ya jinsi hiyo ni ya Msanii gani Tanzania?
01 October 2007
Malkia Nzinga Mbande wa Angola.

Nikiwa katika harakati ya kukusanya habari za wanawake waliotia fora duniani, nimeona niirudishe habari hii niliyoiandika hapo nyuma 2005 wakati nikianza kublogu hii ni kuwapa fursa wale ambao hawakuweza kuisoma nao wapate kumfahamu mama huyu, haya endelea...
Kama ukibahatika sasa hivi kukutana na Mreno, wewe jifanye kama unamchokoza juu ya wanawake wa afrika kwamba hawana lolote na hawawezi lolote, uone atakavyokushangaa, na bila shaka atakutupia swali kwamba unaishi dunia gani wewe?
Wasomaji msishangae, kwani aisifiae mvua...imemnyea. Hii yote imetokana na mwanamke mmoja jasiri, shupavu, mwenye akili sana na asiyetaka kuonewa wala kudharauliwa, si mwingine ni Malkia Nzinga Mbande. Mwanamama huyu aliyezaliwa mwaka 1583 na kufa 1663, alikuwa ni mtoto wa chifu na aliishi kipindi ambacho biashara ya utumwa ndio ilikuwa imepamba moto kwelikweli, kwa bahati mbaya baba yake alifariki na hivyo kaka yake mkubwa bwana Ngola Ngoli Mbandi akarithishwa madaraka ya baba yake. Mm! kaka huyu bila shaka aliguna kwa kujua kabisa kasheshe analotakiwa alikabili la kuwazuia wareno kuingia nchini kwao, lakini afanyeje na yeye ndio mwanaume na kama inavyojulikana kwa wengi mwanaume anaweza kila kitu na daima si mwoga, ikabidi ayavae madaraka huku akijua kabisa yeye ubavu wa kukabiliana na wareno hana na ni
mwoga kufa.
Dada yake, Nzinga baada ya kuona kaka yake anasua-sua ikabidi amwambie, kaka ni lazima uchukue hatua juu watu hawa na kuwazuia kuingia kututawala, lakini kwa vile kaka yake alikuwa mwoga ikabidi amwombe dada yake amsaidie, mara moja bila kuchelewa mwana mama Nzinga akaanza kuchukua hatua za utekelezaji na akafanikiwa kuwashawishi wareno katika kuandika mkataba wa makubaliano ya amani.
Tarehe ikapangwa ya kuweka saini makubaliano hayo, Kaka mtu kwa woga akakataa kwenda hivyo ikabidi Nzinga amwakilishe, akaenda na watumishi kadhaa lakini walipofika ndani ya ukumbi Nzinga akagundua kwamba hakuwekewa kiti yeye kama kiongozi wa nchi yake isipokuwa gavana wakireno peke yake, mwanamama akaona dharau gani hii? mara moja akapiga kofi na mmoja wa watumishi wake akaja mbele yake na kuinama magoti na mikono chini, Nzinga akakaa juu yake, kwa hiyo suala la gavana kukaa kwenye kiti peke yake likawa ngoma droo. Gavana akamtizama yule mama bila kummaliza na kubaki na aibu ya kuzidiwa maarifa tena na mwanamke, bila shaka alibaki akijiambia duh! kumbe wanawake nao wamo!!!
Nzinga baada ya kugundua kwamba kaka yake si kiongozi mzuri na hawezi kila kitu, alimfunga na kujitangaza kwamba yeye ndiye atakayeshika nchi kinyume na desturi ya nchi yao kwamba mwanamke haruhusiwi kushika wadhifa wowote wa uongozi katika serikali, minong'ono ya hapa na pale ilitokea lakini haikufika mbali kwani Nzinga alithibitisha ujasiri wake kwa vitendo. Na ni hapo ndipo umalkia wake ulipoanzia.
Kwa muda wa miaka arobaini ya uongozi wake, wareno walishindwa kuitwaa Angola hadi alipofariki, mwanamama huyu alijulikana na kuogopwa sana na ulaya nzima kwa mbinu zake thabiti za kijeshi, alijulikana kama mwanamke mpiganaji, jasiri na mwenye akili.
Hebu fikiria wareno, pamoja na kuwa na silaha imara na za kisasa ukilinganisha na za Malkia Nzinga, lakini walishindwa kuiteka Angola hadi Malkia Nzinga alipokufa.
Huyu kweli ni mwanamke wa shoka, na nina amini kila mwanamke anaweza kuwa mwanamke wa shoka, pale atakapoamua kufanya jambo kwa moyo na kuondoa uwoga. Hapa duniani kila jambo linawezekana, tatizo liko kwetu sisi wenyewe kutanguliza woga na kutokutaka kusumbuka.
Kama ukibahatika sasa hivi kukutana na Mreno, wewe jifanye kama unamchokoza juu ya wanawake wa afrika kwamba hawana lolote na hawawezi lolote, uone atakavyokushangaa, na bila shaka atakutupia swali kwamba unaishi dunia gani wewe?
Wasomaji msishangae, kwani aisifiae mvua...imemnyea. Hii yote imetokana na mwanamke mmoja jasiri, shupavu, mwenye akili sana na asiyetaka kuonewa wala kudharauliwa, si mwingine ni Malkia Nzinga Mbande. Mwanamama huyu aliyezaliwa mwaka 1583 na kufa 1663, alikuwa ni mtoto wa chifu na aliishi kipindi ambacho biashara ya utumwa ndio ilikuwa imepamba moto kwelikweli, kwa bahati mbaya baba yake alifariki na hivyo kaka yake mkubwa bwana Ngola Ngoli Mbandi akarithishwa madaraka ya baba yake. Mm! kaka huyu bila shaka aliguna kwa kujua kabisa kasheshe analotakiwa alikabili la kuwazuia wareno kuingia nchini kwao, lakini afanyeje na yeye ndio mwanaume na kama inavyojulikana kwa wengi mwanaume anaweza kila kitu na daima si mwoga, ikabidi ayavae madaraka huku akijua kabisa yeye ubavu wa kukabiliana na wareno hana na ni
mwoga kufa.
Dada yake, Nzinga baada ya kuona kaka yake anasua-sua ikabidi amwambie, kaka ni lazima uchukue hatua juu watu hawa na kuwazuia kuingia kututawala, lakini kwa vile kaka yake alikuwa mwoga ikabidi amwombe dada yake amsaidie, mara moja bila kuchelewa mwana mama Nzinga akaanza kuchukua hatua za utekelezaji na akafanikiwa kuwashawishi wareno katika kuandika mkataba wa makubaliano ya amani.
Tarehe ikapangwa ya kuweka saini makubaliano hayo, Kaka mtu kwa woga akakataa kwenda hivyo ikabidi Nzinga amwakilishe, akaenda na watumishi kadhaa lakini walipofika ndani ya ukumbi Nzinga akagundua kwamba hakuwekewa kiti yeye kama kiongozi wa nchi yake isipokuwa gavana wakireno peke yake, mwanamama akaona dharau gani hii? mara moja akapiga kofi na mmoja wa watumishi wake akaja mbele yake na kuinama magoti na mikono chini, Nzinga akakaa juu yake, kwa hiyo suala la gavana kukaa kwenye kiti peke yake likawa ngoma droo. Gavana akamtizama yule mama bila kummaliza na kubaki na aibu ya kuzidiwa maarifa tena na mwanamke, bila shaka alibaki akijiambia duh! kumbe wanawake nao wamo!!!
Nzinga baada ya kugundua kwamba kaka yake si kiongozi mzuri na hawezi kila kitu, alimfunga na kujitangaza kwamba yeye ndiye atakayeshika nchi kinyume na desturi ya nchi yao kwamba mwanamke haruhusiwi kushika wadhifa wowote wa uongozi katika serikali, minong'ono ya hapa na pale ilitokea lakini haikufika mbali kwani Nzinga alithibitisha ujasiri wake kwa vitendo. Na ni hapo ndipo umalkia wake ulipoanzia.
Kwa muda wa miaka arobaini ya uongozi wake, wareno walishindwa kuitwaa Angola hadi alipofariki, mwanamama huyu alijulikana na kuogopwa sana na ulaya nzima kwa mbinu zake thabiti za kijeshi, alijulikana kama mwanamke mpiganaji, jasiri na mwenye akili.
Hebu fikiria wareno, pamoja na kuwa na silaha imara na za kisasa ukilinganisha na za Malkia Nzinga, lakini walishindwa kuiteka Angola hadi Malkia Nzinga alipokufa.
Huyu kweli ni mwanamke wa shoka, na nina amini kila mwanamke anaweza kuwa mwanamke wa shoka, pale atakapoamua kufanya jambo kwa moyo na kuondoa uwoga. Hapa duniani kila jambo linawezekana, tatizo liko kwetu sisi wenyewe kutanguliza woga na kutokutaka kusumbuka.
27 September 2007
Babu Kaduma amefariki dunia.

Babu Kaduma kama wengi tulivyozoea kumwita, hatuko naye tena duniani. Kifo chake kimetokea leo mchana katika hospitali ya Muhimbili alikokuwa amelazwa. Tutamkumbuka sana kwa mchango wake mkubwa alioutoa katika sanaa za maonyesho nchini na nje ya nchi. Mungu amlaze pema Amina.
24 September 2007
Tunaomba mawazo yako.
Wadau, tukiwa katikati kabisa mwa shughuli yetu ya kuunda Jumuiya ya blogu za Tanzania, sasa katiba ya mwanzo au tuseme ya awali imetoka, tunachokuomba ndugu msomaji ni kwamba ipitie uisome kwa makini halafu toa maoni yako juu ya kuibooresha zaidi. Jumuiya yetu inaamini kwamba kidole kimoja hakivunji chawa na ndiyo sababu tukaona haitoshi kwa viongozi peke yake kumaliza kila kitu katika kutengeneza katiba hii, tunaomba sana tena sana tusaidiane katika hili. Karibuni sana, bonyeza hapa uchangie.
Nimerudi..

Sekunde, dakika, masaa, siku na sasa miezi kadhaa imepita tangu da'Mija nitoweke ghafla mtandaoni. Mambo mengi yamepita hapo katikati yaliyonifanya nishindwe kuonekana kama ilivyo kawaida yangu, lakini hata hivyo nashukuru Mungu ameniwezesha kurudi salama salimini kwa wadau wangu.
Naomba nichukuwe nafasi hii kuwashukuruni sana kwa hongera na heri mlizonitakia katika maisha yangu mapya ya familia, Mungu awabariki sana.
Nimerudi jamani
13 July 2007
Nyapara na Manamba.. waraka toka kwa Tungaraza MtiMkubwa.
Siku moja nilipata kuangalia filamu ya maisha ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Marehemu Kapteni Jean Baptist Bokassa. Baada ya kuitazama ile filamu nikashikwa na tafakuri juu ya tabia za binadamu hususani pale wanapokuwa na madaraka.
Jambo moja nililolibaini katika tafakuri yangu ni kwamba wanaadamu wengi wanapenda madaraka. Zaidi ya hivyo madaraka yanaweza kulevya vibaya kuliko pombe kali au bangi. Watu hupata madaraka ama kwa kuzaliwa kwenye koo iliyopo madarakani mathalani wafalme, malkia, masultani na watemi, au kwa taaluma, au kwa kuteuliwa, au kupigiwa kura, au kwa kujipachika, au kwa kunyang'anya, au kwa mizengwe.
Ili kujikweza kimadaraka watu hunakshi nomino zao na badala ya kuitwa majina yao huwa wanaitwa Mtukufu Rais, Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Spika, Waziri, Naibu, Katibu, Mkuu, Mzee, Baba wa Taifa, Ofisa, Dokta, Profesa, Mtakatifu, Mchungaji, Askofu, Muinjilisti, Kateksiti, Maalim, Alhaji, Shehe, Imam, Walii, Maulana, Ayatollah, Chifu, CEO, Mheshimiwa Balozi, Jenero, Afande, Kamanda, Mtaalam, Bwana, Bibi, na kadhalika.
Madaraka humpa mtu uwezo wa kuelekeza muelekeo wa tabia za wale anaowaongoza hali kadhalika mfumo, utaratibu, na muundo wa taasisi anayoiongoza. Madaraka yanaweza kujenga, kubomoa, au kuharibu tabia ya mtu au taasisi. Mifano ya taasisi na watu waliojengwa, kubomolewa au kuhitilafiwa tabia kwa sababu ya madaraka ni mingi sana. Pia madaraka huweza kutukuza au kudhalilisha. Wapo watu kwa sababu ya umakini wao katika madaraka nomino zao zilinakshiwa Utakatifu na wale waliopotosha madaraka yao walinakshiwa Udikiteta au Fashisti.
Madaraka hujenga tabaka la viongozi na maamuma. Mfano wa haya makundi ya viongozi na maamuma ni kama yale wahubiri na waumini, wanasiasa na wananchi, viongozi na wafanyakazi, afande na kuruta, na kadhalika. Kuna wakati utawasikia wale walio madarakani wakisema "..Watu wangu wako wapi?.." "..Vijana wangu wanahitaji..." ...Watu wangu tuliwaahidi kuwajengea zahanati.." na kadhalika.
Wiki kadhaa zilizopita niliandika kuhusu muelekeo wa Mheshimiwa Spika na Naibu wake na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Tanzania la sasa. Ukifuatilia utaratibu wa hoja, maswali, na majibu bungeni hutasita kukubaliwa kuwa bunge letu limekuwa kama la Nyapara na Manamba. Mfano mmoja huo hapo chini:
Spika azuia maswali ya afya magerezani
Basil Msongo, Dodoma
HabariLeo; Thursday,July 12, 2007 @00:04
SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta jana alizua gumzo bungeni baada ya kuzuia Wizara ya Mambo ya Ndani isijibu maswali matatu ya nyongeza kuhusu hali ya afya magerezani ikiwamo Ukimwi na magonjwa mengine ya kuambukiza.
Alitoa uamuzi huo wakati Naibu Waziri, Lawrance Masha akijiandaa kuyajibu baada ya kujibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhonga Ruhwanya (CHADEMA) aliyetaka kujua ni hatua gani zinachukuliwa kuhakikisha Ukimwi hausambai magerezani hasa kwa watoto waliochanganywa na watu wazima kutokana na uhaba wa jela za watoto.
Kabla ya Spika Sitta kuzuia majibu ya nyongeza, Masha alisema si kweli kuwa wafungwa wanaandamwa na maradhi ya kuambukiza magerezani ukiwamo Ukimwi. Akiuliza swali la nyongeza, Mhonga alimuuliza Naibu Waziri endapo atakuwa tayari kubadili kauli hiyo endapo mbunge huyo atampatia ushahidi kuthibitisha kukithiri kwa magonjwa ya kuambukiza magerezani ukiwamo Ukimwi.
Mbunge huyo pia aliuliza ni bajeti kiasi gani imetengwa kukabiliana na Ukimwi magerezani. Hapo Spika akaamuru swali hilo lisijibiwe. Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa (Chadema) alisema, taarifa ya Tume ya Jaji Kissanga ilibainisha kuwapo kwa tatizo hilo katika magereza takriban yote nchini hivyo akaitaka wizara hiyo ieleze endapo taarifa ya tume hiyo si sahihi.
Spika aliamuru pia swali hilo lisijibiwe hali iliyozua gumzo miongoni mwa wabunge hasa wa kambi ya upinzani. Kabla ya uamuzi wa Spika, Masha aliliambia Bunge kuwa serikali imechukua hatua kadhaa kuhakikisha kuwa Ukimwi hausambai magerezani ikiwa ni pamoja na kuzuia aina yoyote ya ngono magerezani na kuwatenga wafungwa na mahabusu wanawake na wanaume.
Kwa mujibu wa Masha, watoto wanatengwa na watu wazima magerezani ingawa Mbunge Mhonga alisema kuna jela tatu tu za watoto nchini, na moja ya vijana. Alisema viwango vya maradhi magerezani si tofauti na katika jamii kwa kuwa katika kila gereza kuna huduma ya tiba kwa ajili ya wafungwa.
Ili kudhibiti magonjwa ya kuambukiza magerezani, askari kusimamia kazi ya kuwanyoa wafungwa na kutaja vifaa vinavyotumika kuwa ni mikasi, nyembe, brashi, mafuta maalumu ya kunyolea na sabuni.
Jambo moja nililolibaini katika tafakuri yangu ni kwamba wanaadamu wengi wanapenda madaraka. Zaidi ya hivyo madaraka yanaweza kulevya vibaya kuliko pombe kali au bangi. Watu hupata madaraka ama kwa kuzaliwa kwenye koo iliyopo madarakani mathalani wafalme, malkia, masultani na watemi, au kwa taaluma, au kwa kuteuliwa, au kupigiwa kura, au kwa kujipachika, au kwa kunyang'anya, au kwa mizengwe.
Ili kujikweza kimadaraka watu hunakshi nomino zao na badala ya kuitwa majina yao huwa wanaitwa Mtukufu Rais, Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Spika, Waziri, Naibu, Katibu, Mkuu, Mzee, Baba wa Taifa, Ofisa, Dokta, Profesa, Mtakatifu, Mchungaji, Askofu, Muinjilisti, Kateksiti, Maalim, Alhaji, Shehe, Imam, Walii, Maulana, Ayatollah, Chifu, CEO, Mheshimiwa Balozi, Jenero, Afande, Kamanda, Mtaalam, Bwana, Bibi, na kadhalika.
Madaraka humpa mtu uwezo wa kuelekeza muelekeo wa tabia za wale anaowaongoza hali kadhalika mfumo, utaratibu, na muundo wa taasisi anayoiongoza. Madaraka yanaweza kujenga, kubomoa, au kuharibu tabia ya mtu au taasisi. Mifano ya taasisi na watu waliojengwa, kubomolewa au kuhitilafiwa tabia kwa sababu ya madaraka ni mingi sana. Pia madaraka huweza kutukuza au kudhalilisha. Wapo watu kwa sababu ya umakini wao katika madaraka nomino zao zilinakshiwa Utakatifu na wale waliopotosha madaraka yao walinakshiwa Udikiteta au Fashisti.
Madaraka hujenga tabaka la viongozi na maamuma. Mfano wa haya makundi ya viongozi na maamuma ni kama yale wahubiri na waumini, wanasiasa na wananchi, viongozi na wafanyakazi, afande na kuruta, na kadhalika. Kuna wakati utawasikia wale walio madarakani wakisema "..Watu wangu wako wapi?.." "..Vijana wangu wanahitaji..." ...Watu wangu tuliwaahidi kuwajengea zahanati.." na kadhalika.
Wiki kadhaa zilizopita niliandika kuhusu muelekeo wa Mheshimiwa Spika na Naibu wake na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Tanzania la sasa. Ukifuatilia utaratibu wa hoja, maswali, na majibu bungeni hutasita kukubaliwa kuwa bunge letu limekuwa kama la Nyapara na Manamba. Mfano mmoja huo hapo chini:
Spika azuia maswali ya afya magerezani
Basil Msongo, Dodoma
HabariLeo; Thursday,July 12, 2007 @00:04
SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta jana alizua gumzo bungeni baada ya kuzuia Wizara ya Mambo ya Ndani isijibu maswali matatu ya nyongeza kuhusu hali ya afya magerezani ikiwamo Ukimwi na magonjwa mengine ya kuambukiza.
Alitoa uamuzi huo wakati Naibu Waziri, Lawrance Masha akijiandaa kuyajibu baada ya kujibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhonga Ruhwanya (CHADEMA) aliyetaka kujua ni hatua gani zinachukuliwa kuhakikisha Ukimwi hausambai magerezani hasa kwa watoto waliochanganywa na watu wazima kutokana na uhaba wa jela za watoto.
Kabla ya Spika Sitta kuzuia majibu ya nyongeza, Masha alisema si kweli kuwa wafungwa wanaandamwa na maradhi ya kuambukiza magerezani ukiwamo Ukimwi. Akiuliza swali la nyongeza, Mhonga alimuuliza Naibu Waziri endapo atakuwa tayari kubadili kauli hiyo endapo mbunge huyo atampatia ushahidi kuthibitisha kukithiri kwa magonjwa ya kuambukiza magerezani ukiwamo Ukimwi.
Mbunge huyo pia aliuliza ni bajeti kiasi gani imetengwa kukabiliana na Ukimwi magerezani. Hapo Spika akaamuru swali hilo lisijibiwe. Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa (Chadema) alisema, taarifa ya Tume ya Jaji Kissanga ilibainisha kuwapo kwa tatizo hilo katika magereza takriban yote nchini hivyo akaitaka wizara hiyo ieleze endapo taarifa ya tume hiyo si sahihi.
Spika aliamuru pia swali hilo lisijibiwe hali iliyozua gumzo miongoni mwa wabunge hasa wa kambi ya upinzani. Kabla ya uamuzi wa Spika, Masha aliliambia Bunge kuwa serikali imechukua hatua kadhaa kuhakikisha kuwa Ukimwi hausambai magerezani ikiwa ni pamoja na kuzuia aina yoyote ya ngono magerezani na kuwatenga wafungwa na mahabusu wanawake na wanaume.
Kwa mujibu wa Masha, watoto wanatengwa na watu wazima magerezani ingawa Mbunge Mhonga alisema kuna jela tatu tu za watoto nchini, na moja ya vijana. Alisema viwango vya maradhi magerezani si tofauti na katika jamii kwa kuwa katika kila gereza kuna huduma ya tiba kwa ajili ya wafungwa.
Ili kudhibiti magonjwa ya kuambukiza magerezani, askari kusimamia kazi ya kuwanyoa wafungwa na kutaja vifaa vinavyotumika kuwa ni mikasi, nyembe, brashi, mafuta maalumu ya kunyolea na sabuni.
03 July 2007
Born Again Pagan anayo haya machache kwa Marehemu Amina Chifupa
Nikiwa mmojawapo wa wanaume Watanzania wapendao kutekeleza na kudumisha mwito wa "kuwawezesha wakina mama na usawa wa jinsia" ("womenn empowerment and gender equality"), napenda sana kutundika katika blog ya "mwanamke wa shoka" katika kumkumbuka Mama Mtanzania, Mbunge, ambaye ametuacha hivi karibuni, kwa shahiri lifuatalo:
Amina Chifupa, Hadithi Yako Itabaki Siku Zote!
Copyright: Born Again Pagan, New York, 2007
Mawinguni yako sauti
Ilitapakaa ki-FM shuti
Kuwatia vijana na watoto buti
Hadithi yako itabaki siku zote!
Ulitekenya fikra za vijana
Kuzipanua bila kubana
Kukubali kushindwa hapana
Hadithi yako itabaki siku zote!
Amina Chifupa ukaingia ndoa
Kwa Mpanganjila bila doa
Wazushi macho kukodoa
Hadithi yako itabaki siku zote!
Amina Chifupa kama dua
Bungeni ulitua
Hoja ya nguvu kutozua
Hadithi yako itabaki siku zote!
Dhidi vilevya jitihada yako
Imehamasisha mapambano
Yaendelea hayo mapambano
Hadithi yako itabaki siku zote!
Wengine vibaya walikuandika
Bloguni nyingi kukubandika
Kwa fimbo kukutandika
Hadithi yako itabaki siku zote!
Kiafya kunyauka kuja
Ukaondoka Dodoma - Lugalo kuja
Hukuachia kutoa hoja
Hadithi yako itabaki siku zote!
Kero wizi wa mitihani
Hukuachia ingawa kitandani
Kupitia kwa swaibu hadi Dodomani
Hadithi yako itabaki siku zote!
Hatujui pengine ulielezeka
Ugonjwa wako kutoelezeka
Kwa wasio karibu kuuweka
Hadithi yako itabaki siku zote!
Siyaoni sasa mabaya yakiandikwa
Na fimbo za udaku kutandikwa
Mazuri tu hubandikwa
Hadithi yako itabaki siku zote!
Kama vyako vilemba
Mazuri yanalemba
Kutoka kila upande kupamba
Hadithi yako itabaki siku zote!
Kama yako mavazi
Mabaya si mema malazi
Pumzika kama bora malezi
Hadithi yako itabaki siku zote!
Mlimbwende Amina Chifupa
Umevunja yetu mifupa
Kutuachia tupu chupa
Hadithi yako itabaki siku zote!
Umetuacha bumbuwazi
Lango kubwa wazi
Kuingia hata udaku-mainzi
Hadithi yako itabaki siku zote!
Maneno ya udaku mzito
Yamekuwa ujauzito
Kuzaa zaidi udaku mzito
Hadithi yako itabaki siku zote!
Amina Chifupa wa Baba
Amina Chifupa wa Mama
Mbunge mpendwa wa Tanzania
Hadithi yako itabaki siku zote!
Amina Chifupa, Hadithi Yako Itabaki Siku Zote!
Copyright: Born Again Pagan, New York, 2007
Mawinguni yako sauti
Ilitapakaa ki-FM shuti
Kuwatia vijana na watoto buti
Hadithi yako itabaki siku zote!
Ulitekenya fikra za vijana
Kuzipanua bila kubana
Kukubali kushindwa hapana
Hadithi yako itabaki siku zote!
Amina Chifupa ukaingia ndoa
Kwa Mpanganjila bila doa
Wazushi macho kukodoa
Hadithi yako itabaki siku zote!
Amina Chifupa kama dua
Bungeni ulitua
Hoja ya nguvu kutozua
Hadithi yako itabaki siku zote!
Dhidi vilevya jitihada yako
Imehamasisha mapambano
Yaendelea hayo mapambano
Hadithi yako itabaki siku zote!
Wengine vibaya walikuandika
Bloguni nyingi kukubandika
Kwa fimbo kukutandika
Hadithi yako itabaki siku zote!
Kiafya kunyauka kuja
Ukaondoka Dodoma - Lugalo kuja
Hukuachia kutoa hoja
Hadithi yako itabaki siku zote!
Kero wizi wa mitihani
Hukuachia ingawa kitandani
Kupitia kwa swaibu hadi Dodomani
Hadithi yako itabaki siku zote!
Hatujui pengine ulielezeka
Ugonjwa wako kutoelezeka
Kwa wasio karibu kuuweka
Hadithi yako itabaki siku zote!
Siyaoni sasa mabaya yakiandikwa
Na fimbo za udaku kutandikwa
Mazuri tu hubandikwa
Hadithi yako itabaki siku zote!
Kama vyako vilemba
Mazuri yanalemba
Kutoka kila upande kupamba
Hadithi yako itabaki siku zote!
Kama yako mavazi
Mabaya si mema malazi
Pumzika kama bora malezi
Hadithi yako itabaki siku zote!
Mlimbwende Amina Chifupa
Umevunja yetu mifupa
Kutuachia tupu chupa
Hadithi yako itabaki siku zote!
Umetuacha bumbuwazi
Lango kubwa wazi
Kuingia hata udaku-mainzi
Hadithi yako itabaki siku zote!
Maneno ya udaku mzito
Yamekuwa ujauzito
Kuzaa zaidi udaku mzito
Hadithi yako itabaki siku zote!
Amina Chifupa wa Baba
Amina Chifupa wa Mama
Mbunge mpendwa wa Tanzania
Hadithi yako itabaki siku zote!
29 June 2007
Usisahau kupiga kura. 29 na 30 June 2007.
Wasomaji wangu ingawa bado tuko katika majonzi mazito ya kuondokewa na kipenzi chetu, lakini tusisahau upigaji kura unaendelea hapa. Swali je umeshapiga kura??
26 June 2007
Katutoka kama mchezo...

Bado siamini kama Mbunge Amina katutoka. Lakini yote tunamuachia Mungu, tunaomba Mungu ailaze roho yake mahali pema, Amina.
20 June 2007
Fide ajisemea.." ..Ukishindwa kukasirika cheka..
Jumamosi iliyopita Watanzania tuligubikwa furaha baada ya timu yetu ya taifa kuifunga timu ya taifa ya Burkina Faso goli 1-0. Nderemo, vifijo, na halahala nyingine za furaha ya ushindi wa Taifa Stars ziliashiriwa kwa namna anuai mojawapo ikiwa ni ya uzuru wa wachezaji wa Taifa Stars bungeni mjini Dodoma.
Katika uzuru huo wa Taifa Stars bungeni Dodoma jumla ya shilingi milion 322.5 zilichangwa kama bahashishi ya wachezaji wa timu ya Taifa Stars. Miongoni mwa wachangiaji walikuwemo Wananchi, Wapenzi wa soka, Vigogo = Waheshimiwa Wabunge na Mawaziri, Wafanyabiashara, pamoja na Wizara mbali mbali.
Moyo huu wa 'harambee' pengine unaweza kukuchekesha au kukukasirisha. Kama UKISHINDWA KUKASIRIKA CHEKA:
The ‘harambee’ continued during luncheon at which Infrastructure Development Minister Andrew Chenge said his ministry and institutions under it were topping up their earlier pledge (70m/-) by 30m/-.
Other pledges were made by Industries and Trade Minister (30m/-), Labour, Employment and Youth Minister John Chiligati (10m/-) while Energy and Minerals Minister Nazir Karamagi pledged 15m/-. He also pledged a further 15m/- from his personal companies.
Singida Urban MP Mohammed Dewji gave 30m/- while the proprietor of TIOT Company pledged 10m/-. Dodoma residents contributed 25m/- on the spot at the airport. Team captain Shadrack Nsajigwa received the money from the prime minister on behalf of his colleagues.
Kwa habari kamili gonga hapa.
Katika uzuru huo wa Taifa Stars bungeni Dodoma jumla ya shilingi milion 322.5 zilichangwa kama bahashishi ya wachezaji wa timu ya Taifa Stars. Miongoni mwa wachangiaji walikuwemo Wananchi, Wapenzi wa soka, Vigogo = Waheshimiwa Wabunge na Mawaziri, Wafanyabiashara, pamoja na Wizara mbali mbali.
Moyo huu wa 'harambee' pengine unaweza kukuchekesha au kukukasirisha. Kama UKISHINDWA KUKASIRIKA CHEKA:
The ‘harambee’ continued during luncheon at which Infrastructure Development Minister Andrew Chenge said his ministry and institutions under it were topping up their earlier pledge (70m/-) by 30m/-.
Other pledges were made by Industries and Trade Minister (30m/-), Labour, Employment and Youth Minister John Chiligati (10m/-) while Energy and Minerals Minister Nazir Karamagi pledged 15m/-. He also pledged a further 15m/- from his personal companies.
Singida Urban MP Mohammed Dewji gave 30m/- while the proprietor of TIOT Company pledged 10m/-. Dodoma residents contributed 25m/- on the spot at the airport. Team captain Shadrack Nsajigwa received the money from the prime minister on behalf of his colleagues.
Kwa habari kamili gonga hapa.
13 May 2007
Nani kama mama?
Leo ni siku ya mama, tusaidiane kumsikiliza mzee Nico Mbarga halafu utaniambia mwenyewe.
07 May 2007
Bongo Niu Yoki...
Habari hii chini inaletwa na mwanaharakati MtiMkubwa...haya endelea.
Mambo ya Bongo sasa hivi kiboko; kuna mashopingi moli kama ya mtoni, Maubungo Plaza, Mayfair Plaza na maplaza mengine mengi tuuu! Maapatimenti, mariili esteti broka, mabangaloo, na maskai skrepa! halafu mabarabara ya kimtoni na madaraja kama lile la Kibiti watasha wenyewe wanabloo! Na neshino stediumu mpya ikiisha litakuwa hamna tena Afrika nzima!
Mademu siku hizi wanang'aaaa! Kuna maMiss kata, miss tarafa, miss wilaya, miss mkoa, miss Tanzania, mpaka miss yunivasi! Mafasheni shoo, madizaina, na mamodozi! Maselebriti wa vipaji vya kitaaluma, kisanii, kimichezo, kisiasa, ua kwa majina ya ukoo. Kuna Matamasha, mabonanza, na makonseti hatari tupu!
Redio stesheni za kumwaga siyo kama wakati ule idhaa tatu tu; taifa, biashara na eksteno sevisi iliyokuwa inafunguliwa kwa masaa maalumu na kipindi kimoja tu c
Mambo ya Bongo sasa hivi kiboko; kuna mashopingi moli kama ya mtoni, Maubungo Plaza, Mayfair Plaza na maplaza mengine mengi tuuu! Maapatimenti, mariili esteti broka, mabangaloo, na maskai skrepa! halafu mabarabara ya kimtoni na madaraja kama lile la Kibiti watasha wenyewe wanabloo! Na neshino stediumu mpya ikiisha litakuwa hamna tena Afrika nzima!
Mademu siku hizi wanang'aaaa! Kuna maMiss kata, miss tarafa, miss wilaya, miss mkoa, miss Tanzania, mpaka miss yunivasi! Mafasheni shoo, madizaina, na mamodozi! Maselebriti wa vipaji vya kitaaluma, kisanii, kimichezo, kisiasa, ua kwa majina ya ukoo. Kuna Matamasha, mabonanza, na makonseti hatari tupu!
Redio stesheni za kumwaga siyo kama wakati ule idhaa tatu tu; taifa, biashara na eksteno sevisi iliyokuwa inafunguliwa kwa masaa maalumu na kipindi kimoja tu c