Swali linalobeba kichwa cha habari hii lililetwa na bwana Ramadhani Msangi ambaye naye alilipata kutokana na habari iliyoletwa na bwana MtiMkubwa inayosema.. "Aliyenacho ataongezewa..."
Habari hii imezua mjadala mkubwa juu ya nchi yetu na ulinzi wake, juu ya uzembe unaochukuliwa na viongozi mbalimbali duniani hata kama wanapata tahadhari ya uvamizi wa kigaidi. Mijadala ya namna hii mimi huipenda kwa vile huibua mambo ambayo labda hata hatukuwa tukiyafahamu. Ndugu zanguni hili swali la Msangi Mdogo kwangu mimi nalitafsiri kama kwamba hali hii tumeona haiwezekani tena kubadilika, ni kama tumeihalalisha vile... hebu tusome kwanza haya maoni yaliyoletwa na baadhi ya wasomaji halafu tuendelee kutafuta ufumbuzi....kwa kweli halali mtu hadi kieleweke...
MK ...... Kwanza kabisa nakuunga mkono ndugu muandishi wa hii nakala kwa yale yote ya kweli uliyo yasema hapa.
Tanzania na nchi nyingi za Africa mara nyingi hawafuati sheria na katiba za nchi zao kwa kutenda haki kwa raia wao. Ikitokea Kiongozi yoyote yule kusema lolote ili mradi matakwa yake yafuatwe basi kweli lolote lile litatendeka ata watu kufa watakufa.
Ktk nchi yetu ya Tanzania mtu ukiwa masikini basi haki zako zile za msingi utazikosa kwa kunyanyaswa kila kona toka kwa majirani zako, kutoka ktk vyombo vya ulinzi, kupata huduma ktk ma-hospitalini, makazini na mashirika ya umma. Hii imeoneshwa mara kwa mara kwa baadhi ya wanajeshi wetu kupiga raia pale wanapojisikia au kwa kitendo hicho kilichotokea na watu kufa.
Ktk yale yote yaliyotokea na watu wawili kufa ni uzembe wa Serikali yetu kwa kutotoa (kuto-kutengeneza) nafasi nyingi za kazi kwa raia wote ndani ya nchi. Kama kila raia angekuwa na kazi itakayo muezesha kupata ridhiki yake basi haya yasingetokea kwa maana hawa ndugu zangu wangekuwa na mahali pa kufanyia shughuli zao na kujipatia riziki.
Kama haiwezekani kwa kila mtu kupata kazi basi kwanini hawa watu wasiweze kuhalalishwa na kuendelea na kazi zao kama wapiga debe.
Serikali haitoi kazi kwa raia lakini utakuta kila siku wanawasumbua wamachinga ambao wamejitaidi na kujianzishia maisha yao kwa kufanya biashara!Kweli hii inatia hasira sana.
Sijui wana maanisha nini kwa raia! Mimi sio siri nina kerwa sana na mengi yatokeayo Africa na Tanzania.
Baadhi yao hawawezi kuelewa haya mambo (shida) maana wao wamejilimbikizia utajiri mwingi kutokana na rushwa na kuiba pesa za Taifa.Ukweli na ushaidi upo!!
Wengi wa Viongozi wetu hawapo ktk kulitumikia Taifa na wananchi wake bali wapo kama ktk Biashara ili wajitafutie utajiri wao na familia zao na hii imeoneshwa kwa wao kununua nafasi za kugombea Ubunge au kila siku kugombea nafasi moja tu, n.k. na kutoa rushwa kwa raia ili wachaguliwe na wengine ata kuiba kura.Ukweli umeoneshwa kwa wao kuomba kuongezewa mishahara.
Kwa kweli inatia hasira sana, Cha msingi na la maana ni kwa mimi na wewe (wasomaji) kuweza kugombea hizo nafasi zao ili tuweze kusimama na kutetea masilahi ya Taifa na wananchi wake.
Kama mnataka mnabidi mpitie CCM maana kama ukienda Upinzani ni kama unajipotezea muda wako maana wapinzani wote ni kama CCM Pretenders wanao danganya raia.Ushaidi upo!
Kuhusu jeshi kunyanyasa raia hawawezi kulizungumzia hili swala maana wengi wa Viongozi wanaogopa kupinduliwa!
Tanzania kuwa kama Wasierra Leone au Waliberia au nchi kupinduliwa kutokana na wananchi ni Vigumu sana tena sana maana kuna watu wapo masaa 24 ktk kulinda nchi hii. Labda itokee kwa genelari wajuu sana kufanya hivyo na vile vile ni vigumu maana wanajeshi wote wenye vyeo vya juu waliostaafu na wale wapo kazini wanafuatiliwa mienendo yao ya kila siku in details hivyo itajulikana tu kabla ya wao kufanya hivyo.
Kingine vyombo vyetu vya Ulinzi vinapata mafunzo toka Canada, China, USA, UK na kidogo Russia, na nchi zinginezo hivyo wao utoa mafunzo ya hali ya juu ya kuzima mapinduzi ktk nchi kwa maana hiyo ata kama yakitokea nina uhakika zaidi ya asilimia mia mbili (200) yatazimwa chini ya masaa 24.
Ninacho mshukuru Mungu Taifa letu limebalikiwa na Amani ambayo itadumu milele. Kingine, Amani ndio itakayo fanya mimi na wewe au kizazi chetu kiendelea hivyo tudumishe Amani yetu tuliyo nayo.
Ingawa kuna Viongozi wabaya lakini kuna wengi wazuri.Inatia hasira sana lakini tuwe na moyo na JKM maana kuna mengi yatakuja na haya yaliyotokea hayatatokea tena.
Nadhani sitokuwa nimewaudhi baadhi ya wasomaji wengine, Kama mtakuwa mmeudhika kwa yote nawaomba mniwie radhi.Ukweli utabaki ukweli.
michuzi...... naomba nichangie kwa kuwa sina upande katika suala hili, kwani kwa mujibu wa maono yangu, nadhani kila upande unastahili lawama.
nikianza na serikali: hivi kuna ubaya gani kuweka sera ya wazi kuhusu biashara ndogondogo na wafanyaji wake? Kuna ubaya gani kuiga wenzetu ughaibuni kwa kutenga sehemu maalumu za kufanya biashara hizo, na sehemu hizo ziwe zinafikiwa kirahisi na sio kama hivi sasa pale karume ama mwenge. nimeona sehemu kama stockholm wana soko la mchana katikati ya jiji, helsinki pia, berlin nimeona pia hali kadhalika london na johannesburg, kuna masoko ya mchana kwa holoi poloi, lakini hakuna ruhusa kufanya biashara popote kama ilivyo dar, kiasi inatia kinyaa.
Kwa machinga: hivi nani kawaambia kuwa mradi wao walipiga kura kuitia ikulu serikali iliyo madarakani maana yake wafanye watakavyo hata kama ni kinyume cha kanuni? kwa nini wanakuwa wabishi na kuwafanya halmasahuri ya jiji waonekane wanawaonea, kuchoma chipsi na kuuza mashati kila sehemu katikati ya jiji? ni kweli wote wanastahili sehemu kufanyia bizness, lakini ni kila sehemu jamani? mtimkubwa na wengineo hebu rudini muone ilivyo shida kukatiza mitaani dar kutokana na vibanda vya biashara na machinga. sisemi nawachukia,ila kama ni maendeleo yaje kwa nguvu za hoja na sio hoja za nguvu kama anavyotoa mtimkubwa.
nasema haya sababu hata hii serikali imeyaona hayo na ndo maana imesitisha (haijakatisha) kwa muda wa miezi 6 zoezi la safisha jiji, ila baada ya hapo hakuna maslie. lazima barabara iwe barabara na vibaraza viwe hivyo. we umeona wapi chupi zikauzwa kwenye kibanda cha kituo cha basi? sipendi kuweka picha kama hizo bloguni
kwani nadhani si vyema kila mtu duniani akaona aibu yetu.
F MtiMkubwa Tungaraza...Muhidin,
Maelezo yako yamenikumbusha fasihi ya kidato cha tatu kitabu cha Ngugi wa Thiongo, This Time Tomorrow. Aibu ya serikali ni kuwa na wauza vyupi katikati ya jiji! Hii mipango ya kuwakarahisha wananchi haikuanza leo: wengi wetu bado tunakumbuka sana halahala za polisi, mgambo, na JKT wakati wa zoezi la kuwahamisha "wazururaji" toka Dar es Salaam kwenda Geza Ulole, Kibugumo, Mwanabilato, Chanika, Chamanzi, Msanga, Mkuranga, Kigamboni na kwingineko koote kwenye makao mapya. Baada ya zoezi hilo likaja zoezi la NGUVU KAZI wananchi wakakarahishwa tena. Akitokea mchunguzi wa mambo ya kijamii (social researcher) kuja kufanya tathmini ya miaka ishirini hadi thelathini baada ya mazoezi hayo sijui kama kutakuwa na matokeo ya mafanikio.
Uchafu kwa fasili yake ni kitu chochote kilichopo mahali pasipohusika. Kama kweli tunataka kusafisha jiji letu kwanza tuanze na kujenga tabia ya usafi miongoni mwetu (personal hygiene). Usafi huu utafanikiwa kwa kuwa kila Mtanzania kujua maana afya bora; kuwa na uwezo wa kula vizuri, kunywa maji safi, kulala mahali pazuri, kuvaa nguo na viatu vizuri, kuweza kununua mswaki na dawa yake. Haya yote yatawezekana ikiwa kama kutakuwa na na uwezo wa kila Mtanzania kuwa na kipato cha kutosha kukidhi mahitaji yake ya kila siku. Kiapto hiki kitapatikana ikiwa tu kama tutaweza kubuni na kuendeleza ajira.
Halafu tukimalizana na suala la usafi binafsi tushughulikie usafi wa mazingira yetu (environmental cleanliness). Uchafu wa mazingira si tu kuwepo kwa Wamachinga katikati ya jiji pia kuwepo mifugo kama kuku, bata, ng'ombe, nguruwe, mbuzi na kondoo katika maeneo ya wanayoishi watu. Nadhani kwa upande wa ufugaji wa wanyama kama ng'ombe, mbuzi, nguruwe na kondoo haupo mitaa ya Kariakoo, Ilala, na Temeke bali Kimara, Mbezi Shamba na Mbezi Beach, Oyster bay, Msasani, Masaki ya Uzunguni siyo Uzaramoni, Kinondoni, Upanga, Sea View, na Mikocheni zote mbili A na B. Hapa ndipo utakapoona aliyenacho ataongezewa. Mkurugenzi wa Jiji ukimshauri atume vijana wake wakabomoe mabanda ya mifugo yaliyopo hizo sehemu nilizozitaja ndipo utakapojua makali na ubutu wake upo wapi.
Hoja ya nguvu na nguvu ya hoja. Nakumbuka katika masaili fulani Bob Marley alisema "..facts 'n' facts is whole lotta o' bullshit.." Wamesitisha na hawakukatisha. Sawa! Kwa nini kabla ya kufikia hatua ya kutekeleza hilo zoezi hawakutathimini mazuri na mabaya yake (pro and cons)? Wanaelimu ya jamii (sociologists), wachumi (economists), au washauri wengine wowote wa serikali wa mambo ya jamii hawakushirikishwa kuitahadharisha serikali juu ya intended consequencies, latent consequencies, na unintended consequencies za zoezi hili?
Rais Nelson Mandela kwenye shajara yake ya Long Walk to Freedom anasema "..ukitaka kuijua serikali nzuri usiangalie inahusiana vipi na raia wake wa juu bali angalia jinsi inavyohusiana na wafungwa wake walio jela.." Haya mambo ya kuikimbiza na kubomoa biashara za watu mijini ni uonevu, unyanyasaji, na dhuluma dhidi ya Watanzania masikini. Kama kweli kuna zoezi la safisha jiji basi lisiwaache na wafugaji wa Oyster Bay, Kinondoni, Ada Estate, Regent Estate, Upanga, Sea View, Mikocheni A na B, Msasani Peninsula/Masaki, Mbezi zote mbili, Kimara, na kwingineko kokote kusikostahili kuwepo mifugo.
Mungu Ibariki Tanzania,
KABLA SIJAACHANA NAWE NAOMBA UIMBE KWA SAUTI WIMBO HUU WA MAREHEMU MAKONGORO:
"Mpango wa pili wa maendeleo umesema kuleni kuku, mayai, mboga, samaki, maziwa, na kujenga nyumba safi pakulala pawe bora!"HAYA YOTE YATAPATIKANA VIPI SIJUI?
John Mwaipopo... Awali ya yote nilidhani wasafwa wako Mbeya kumbe wako Kilombelo (mchomekeo tu msijali sana)
Pili nichangie kidogo juu ya maslahi ya wabunge na madaktari. Mosi vyombo vya habari vilitupotosha kuhusu hili. Ingawaje sikubaliani na mapendekezo yao ya kutaka kupanuliwa maslahi, vyombo ya habari vilichukulia lile suala kama kikao rasmi ambacho kilikuwa na ansard na minutes. Kumbe yale yalikuwa mawazo ya wabunge binafsi wawili au watatu. Pengine miongoni mwa wabunge wapo ambao walikuwa na mtazamo tofauti. Wanamtandao wakaleta kwetu kana kwamba lile lilikuwa azimio la wabunge woote - Irresponsibe journalism.
Hata hivyo wabunge kama watanzania wengine walikuwa na haki ya walau kuyasema wanayostahiki kuyasema.Madaktari nao walikuwa na haki kudai walichokuwa wakidai. Kosa lao lilikuwa approach. How come wasababishe vifo kwa kugoma kufanya kazi. Ukiwa muhandisi unafikiri kila tatizo linatatuliwa na nyundo. Sivyo. Serikali ilikuwa sahihi kuwaadabisha kama ilivyofanya. Kwa nini hawakutumia power of compromise from different angles. Kizuri hapa hata serikali ilikuwa inatambua madai yao kuwa ni halali. They had no right to cause deaths to innocent and poor patients. Who stopped them from going anywhere around the world to seek greener pastures? Hapa inakuonyesha walikuwa wanatikisa kibiriti tu huku fika walikuwa wanaujua uwezo wa serikali yao.
Michuzi umechambua pande mbili ki ufasaha sana. Huria si holela.Really wamachinga are causing nausea in the 'beautiful' city. Lakini wa kulaumiwa sana hapa ni Serikali, na katu si hawa holoi poloi (asante kwa msamiati huu). Imekuwa iki-react too slowly and unprofessionally. Yenyewe ndio inatakiwa iwe chachu ya uendeshwaji wa shughuli zoote nchini. Mathalani kuhusu suala hili ingeweza kuweka kodi kubwa kwa wafanyabiashara wakubwa wa city centre wanaouza bidhaa sawa na zile za wamachinga. Hii ingewafanya ama waache kufanya biashara hii au ama wafanye kwa asara zao. In the meantime, wamachinga ambao wangetengewa sehemu inayofikika wangeondolewa ama kupunguziwa kodi. Niambie mnunuzi asingeweza hata kwenda mathalani Jangwani (sio kwa Yanga).
Suala ninalolipigia upatu na chapuo bila kusita ni hili alilolileta Mti Mkubwa Mkavu Mnene. Safisha safisha ikirejea ianzie kwa wafugaji wa ng'ombe na mbuzi wa Mbezi beach, Masaki, O'bay na Sea View. Mpango wa kuonea samaki wadogo ufe.
mark msaki nianze na bwana MK usiogope habari ya kufundishwa Urusi. inapokuja suala la living and death, hapo hakuna shule inayotumika. tunapoona nchi zimekuwa na migogoro miaka nenda miaka rudi haina maana kuwa hazikuwa trained kwenye system zake za usalama...unapoongelea suala la amani sijui uko serious au unakoleza mada! hakuna amani kwenye njaa...tuendako ni kwa kuwa makini zaidi maana utandawazi hauruhusu kucheza bao na kupata chakula!! unatoka mzigoni, unapita dukani kununua msosi wa siku hiyo...funga kazi.
Michuzi umesema ukweli na umekuwa fair kuongelea pande zote mbili. kuna swali moja waliuliza juzi wana ?DHW "hivi mnakuwa mmejichimbia wapi?" mtu kupandisha maghorofa wakati maafisa wa ardhi wa sehemu husika wapo...... au kuacha watu wajenge vibanda ili uje wafukuze baadaye...hii kimsingi kwa sehemu kubwa huainisha serekali isiyowajibika...
Mti mkubwa ambao ni mkavu ameainisha kila kitu. kurudia ni kujaza ukumbi wa Da mija bure!! kwa kuongezea mimi ninaona ni ajabu kweli kuwa kila mtu anataka kujibanza DAr...mbona hao wamachinga wakionekana mkoani ni dili? kuna kitu si sahihi - (naona Jk ametoa changamoto Arumeru kuwa mikoa ya pembezoni iangaliwe)....
Mwaipopo mengi ya msingi umeyasema..lakini ukiangalia kiundani zaidi, haina maana kuwa ng'ombe anayekupa maziwa zaidi ndio umuhukumu majani kidogo zaidi...reaction ni reaction...sema matokeo yake ndio huwa tofauti..ina maana mfano kama wabunge wangegoma asingekufa mtu...kufa mtu kwa mgomo ni gauge ya kuonyesha kuwa hiyo fani ni sensitive....japo sisemi kuwa nyengine sio, lakini sensitivity hutofautiana. sipingi maslahi ya wabunge, lakini pia siri ya kuwasahau watendaji pia ni ya kujibu....nimeona waheshimiwa wabunge wameliona hilo na juzi walipigia kelele hazina kulikoni na maslahi mabovu!!! myonge mnyongeni lakini haki yake mumpe....ukichunguza sana suala la wabunge na maslahi lilikolezwa na la ishu ya madaktari ambayo ilitugusa wengi lakini tukabaki kuugulia na kulalama.....
Mk... Ndugu Mark Msaki sio kwamba naogopa kufundishwa Russia bali hii ndio facts ambapo ukweli wake utaoneshwa pale hilo tukio likitokea.
Vyanzo vya ulinzi vinavyolinda Taifa hili vina macho makubwa ndani ya nchi na nje ya nchi sasa sijui hizo silaha utazipitisha wapi kufanya mapinduzi hayo?
Au wananchi kutumia silaha za jadi ambapo watatwaa eneo gani na kusema ndio nchi wamechukua?
Wanajeshi wetu wapo tayali ktk matukio kama hayo ambapo narudia tena nina uhakika wa zaidi ya asilimia mia mbili (200) yatazimwa chini ya masaa 24.
Nadhani bwana Michuzi atakuwa na marafiki zake wengi wa namna hii (wanao linda taifa hili ndani ya nchi na nje ya nchi) ambapo ukiwauliza watasema kama ninavyosema.(Inategemea maana kazi hii ni kama mtoto, unakula kutokana na umri wako = Unajua mengi kutokana na nafasi yako na kitengo chako)
Mataifa mengi ya Africa unayo yaona yana matatizo ya Vita, Sio kwamba Vita hiyo imeanzishwa na mtu mmoja bali imeanzishwa ktk kushirikiana na Mataifa mengi zaidi ya Africa na ya nchi za nje kwa kudhaminiwa kipesa, wanajeshi (watu kufundishwa na ata kununua au kukodisha wanajeshi wale waliostaafu kutoka ktk Mataifa mengine mengi ya Africa), silaha n.k.
Naomba angalia hili swala kwa undani zaidi utaona ninayo sema.
Mfano: Sir Mark Thatcher na mataifa mengine yaliyotaka kuleta mapinduzi Equatorial Guinea lakini kutokana na Good Intelligence report iliyopatikana kutoka kwa mataifa mengi mbalimbali ya Africa yaliweza kutoa habari kwa Serikali za South Africa,Equatorial Guinea,Zimbabwe, na mengi yaliwezesha kwa Sir Mark Thatcher na wenzake wote kukamatwa na mapinduzi kuzimwa kabla ya kutokea.
Sasa Tanzania tuna macho ya kuona Adui kama Binadamu na Adui kama Taifa lolote litakalo kuwa na mawazo ya kupindua nchi yetu na pale tunapofahamu tunazima hiyo mission yao kabla ya tukio kutokea.
Ndio maana ninakwambia Taifa letu kutokea mapinduzi ni vigumu sana, Hii sio kwamba ninazungumza kufurahisha jamii au kukoleza mada la hasha ninazungumza kwa kile ninachokijua kwa undani zaidi.
Tanzania ni moja ya mataifa ya Africa yaliyokuwa na watu waliokuwa na mafunzo ya namna hii (ya hali ya juu) pamoja na jinsi ilivyotawanya macho yake ktk kulinda Taifa hili Kubwa la baadae ulimwenguni.
Mwisho, Vita zote unazoona Congo, na mahali popote pale Africa ni mikono ya Mataifa mengine ya Africa, Mataifa mengine nje ya Africa kupitia raia wa ndani wa nchi husika na wakimaliza wanachotaka toka kwako (Interests kuisha) wanakuua au ku-support mtu mwingine na Vita inaendelea tu upya.
Nadhani sitokuwa nimewaudhi baadhi ya wasomaji wengine, Kama mtakuwa mmeudhika kwa yote nawaomba mniwie radhi.Ukweli utabaki ukweli.
ndesanjo...Kuna jambo Mti kasema aliulizwa na ofisa wa sirikali. Ofisa huyo alitaka ushahidi wa unyama na ukiukwaji wa haki za binadamu. Watwawala wetu wanapenda sana kukimbilia hilo neno, "ushahidi." Mkapa kuna wakati aliviambia vyombo vya habari/uongo vitoe ushahidi kuwa sirikali yake ina wala rushwa. Kitendo cha kiongozi wa sirikali kutojua kuwa vyombo vya dola Tanzania mara nyingi hunyanyasa wananchi na haki za msingi hukiukwa bila woga wowote kinaonyesha kuwa huyo bwana anatakiwa aongozwe na sio aongoze. Hata Mkapa nilimshangaa sana...rais mzima hajui kuwa amezungukwa na wala rushwa anataka wandishi wa habari wampe ushahidi. Keleuwii!
Ramadhani Msangi...
Lakini hii si ndio Bongo jamani??
F MtiMkubwa Tungaraza...MK,
Nashukuru sana kwa maoni yako.
Imani ya kwamba pale nyumbani pako salama na pana walinzi ni nzuri lakini tusilale mlango wazi. Nina maana hata kule kwenye vyombo vya usalama vyenye nguvu na ujuzi kuliko vyetu imewezekana kufanya matendo ya kigaidi na kuingizwa silaha! Kwa mifano hai ni September eleventh, milipuko ya mabomu ya IRA, milipuko ya mabomu Israeli, Moscow, Madrid, Ufaransa na kwingineko sembuse Tanzania ambako kitengo cha makonteina bandari kimebinafsishwa pia tumezungukwa na vita Uganda, Burundi, na Kongo. Kongo inaweza kuwa bonge la kichochoro cha kupitishia silaha kuingia Bongo!
Audhu billah hima shetani rajimu, Allah karim! MUNGU ilinde Tanzania.
MK said... Ninafuhahi kwa kuweza kubadilishana haya mawazo ya ukweli bwana F MtiMkubwa Tungaraza.
Tuanzie 9/11, Kabla ya kumaliza muda wake wa Urais bwana William Jefferson "Bill" Clinton aliweza kupelekewa memo toka CIA na FBI ya kwamba ndani ya USA kuna uwezekano wa kutokea shambulizi kwa kutumia ndege.
Pia CIA iliweza kuitaharifu FAA (Federal Aviation Administration) kuhusu hili swala lakini kutokana na uzembe mmoja au mwingine walipuuza.
Kingine wakati ule CIA na FBI walikuwa hawana uhusiano mzuri wa kubadilishana habari na hivyo kushindwa kuzima hilo tukio.Matokeo yake baadae kiliundwa kitu kinachoitwa Homeland Security chombo kinachoweza kujumuisha intellegence oficials wote toka ktk vyombo vyote ndani ya USA.
Kwasasa hivi anga na Bandari za USA zinalindwa masaa 24 pia kwa ku-scan kila nyumba kuweza kujua kama kuna watu wenye kuleta ujuma.Pia Asilimia kubwa za Computers, simu za ndani ata mobile wana zi-bug ili kusikiliza simu zote za ndani na nje ya USA.
Kwa kifupi 9/11 kilikuwa kitu kinajulikana bali ni uzembe tu wa kiubindamu ulio fanya kutokea.
Mungu awalaze mahali mema peponi Amina wale wote walio patwa haya matatizo.
Kuhusu swala la Israel ni gumu sana maana kuna mataifa toka nje yanayo dhamini hao magaidi na kuua roho za watu wasiokuwa na hatia.Na ndio maana mara kwa mara Israel imeweza kuyashambulia hayo mataifa kwa maneno na Kijeshi.Mataifa hayo ndio juzi tu walimuua waziri mmoja ndani ya nchi moja iliyo karibu na Israel ili nchi hiyo isiwe na Amani (Irudie vita). Sitaki ni yaseme hayo mataifa hapa.
Kuhusu mabomu Moscow ni magaidi wanao toka Chechnya wanafanya hivyo kwa madhumuni ya kuendeleza propaganda ya hiyo state ili iweze kujitenga toka Russia. Kumbuka mwaka 1991 wakati USSR ilipo vunjika mataifa mengi ya muungano yalijitenga ikiwemo Chechnya lakini Russia imekataa kwa hilo swala na mpaka sasa hakuna Taifa linalotambua Chechnya kama nchi bali inatambuliwa kama moja ya state ndani ya Russia.
Ufahamu ya kwamba hawa ni magaidi ambao wengine wanatoka nje nchi na kuingia Chechnya pia wanao husika sio kikundi cha watu mia au elfu moja bali ni watu wengi sana ambapo wana pesa, Silaha na n.k na pia wanapata pesa toka kwa watu au mataifa mengine yanayotaka Russia ipungue nguvu.Russia haiwezi kukubali hili swala kutokea ndio maana serikali ya bwana Vladimir Vladimirovich Putin inapeleka majeshi na ata kuweka budget kupigana hii vita kulinda ardhi yake isipotee kama ardhi nyingine zilizopotea mwaka 1991(Armenia, Azerbaijan, Belarus, Georgia, Kazakhstan, Kyrgyzstan, Moldova, Russia, Tajikistan, Ukraine, Uzbekistan na Turkmenistan).
Nina uhakika Russia itashinda vita hii kwakuwa nguvu wanayo, sababu wanayo na silaha wanazo.
Kuhusu Madrid, Kwanza naomba nikueleze ya kwamba Tarehe 24/03/2006 ETA imeweza kuweka mkataba wa amani na Serikali ya Spain.
Ktk matukio mengi unayo yaona yantokea ni kwamba habari ya tukio husika uwa infahamika bali kuna uzembe utokea. Vyanzo vya Ulinzi vya Spain vilipata hii habari toka kwa mataifa ya Morocco na Egypt lakini kuto-act haraka na mapema ndio inatokea hao magaidi kulipua. Lakini SIO kwamba wamechukua nchi bali ni kuua watu wasiokuwa na hatia.
Narudia tena, Mungu aweze kuwaweka mahali pema peponi amina wale wote walio kumbwa na mikasa hii ktk hii dunia.
Kuhusu the Provos au jina lingine PIRA (The Provisional Irish Republican Army) wengi wanajua kama IRA ni kundi lililo kuwa linataka kuondoa utawala wa mwiingereza ndani ya Northern Ireland na ndani ya United Ireland.
Kutokana na mawazo yao walidhani ya kwamba watashinda malengo yao kwa kutumia Vita, Lakini July 2005 Dunia nzima imeshuhudia tukio la wao kuacha kutumia Vita (silaha za moto) kama suluhisho ya matakwa yao na kusalimisha silaha zao kwa Serikali ya Uingereza.
Hii ni moja ya Ushindi kwa Serikali ya Uingereza na kwa wale wote wapenda Amani duniani nikiwemo nafsi yangu.
Kuhusu kitengo cha makontena ktk Bandari ya nchi yetu kubinafsishwa usiwe na shaka maana sio kwamba tumewapa haki zote kwasababu kama Taifa tutabaki na asilimia za share ktk hiko kitengo au twaweza kutafuta watu watakao fanya kazi ktk kitengo hiko na kuwakilisha Taifa kwa kila details za kontena na mizigo yote inayo ingia ndani ya nchi na kutoka nje.
Pia kabla ya kubinafsishwa tutaweza kuangalia wale wote walio peleka maombi ya ku-take over na watachambuliwa kwa makini.Pia watu wataajiliwa iwe mfanyakazi wa kawaida au Ma-Boss wa juu watakao fanya kazi kama Spooks ili kupata habari na Taarifa zaidi za kila siku hapo bandarini.
Hii ni kitu cha kawaida kwani mbona USA hii imetokea P&0 imenunuliwa na United Arab Emirates (kampuni inaitwa Dubai Ports World), P&O ilikuwa shirika mali ya uingereza na ilikuwa na tender ya ports zote za USA (New York, Newark, Philadelphia, Baltimore, Miami na New Orleans) lakini United Arab Emirates imenunua P&O ( Peninsula and Oriental Steam Navigation Company) sasa kazi zote zitafanywa na Dubai Ports World.Ingawa hili bado linazungumziwa na Congress na Senate.
Ni lazima tuwe na wasiwasi na Congo, Uganda, na Burundi lakini:
Burundi - Vita siku hizi hakuna bali kuna vikundi vidogo vidogo.Kwa ujumla Vita imekwisha.Kwanza Burundi ni kama mikoa miwili ya Tanzania hivyo technically hawawezi kupigana na sisi na kingine kupindua nchi au nchi kuwa na machafuko na kuwa na dalili za Amani kupotea inabidi kuwe na Silaha nyingi za kuleta mapinduzi hivyo ni vigumu kwa kiwango hicho kuingia nchini kirahisi.
Congo - Machafuko yapo lakini majeshi toka UN yatapelekwa kuleta amani.
Uganda - Museveni Huyu bwana ni diktekta kwa kukaa madarakani miaka Ishirini (20)pia anasamehewa madeni na kupewa mikopo yeye anapeleka kununua ndege za kijeshi Israel.
Kuna machafuko ya LRA (Lord's Resistance Army)kundi linalo ongozwa na Joseph Kony ambaye anapata udhamini toka sehemu mbali mbali ndani ya Africa na nje.
Kwa ufupi mapinduzi hayawezi kufanyika Tanzania. Pia toka tukio la kulipuliwa DSM hali ya Ulinzi wa Taifa umeongezeka mara dufu.
Naona niishie hapa maana nimeandika mengi sana.
Nadhani sitokuwa nimewaudhi baadhi ya wasomaji wengine, Kama mtakuwa mmeudhika kwa yote nawaomba mniwie radhi.Ukweli utabaki ukweli.
F MtiMkubwa TungarazaMk,
Asante kwa ujumbe wako.
Awali kabla sijaendelea sana naomba unielewe kwamba nilichozungumzia siyo mapinduzi au machafuko nchini Tanzania. Nilichozungumzia ni tahadhari juu ya kutengeneza watu watakaoweza kuwa waasi kwa sababu za kisiasa, kijamii, na kiuchumi.
Kwa kifupi tu mimi ninafanyakazi na watu waliotoka nchi zilizoathirika na vita. Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana sababu zilizosababisha vita nchini kwao na nani wanaoshiriki katika kupigana vita. Kwa ufupi huwa wananiambia vita vyote vinatokana na kupunjana kiuchumi, tofauti ya itikadi za kisiasa. Pia kwa sababu za kijamii kama ukabila, dini, na rangi. Halafu kuhus kina nani wanaoshiriki kupigana vita huwa wananiambia ni wavulana na wanaume vijana wasio na kazi na wenye elimu ya chini na wanaume wenye umri wa makamo kati ya miaka 35 na 45!
Jingine, ulipozungumzia Chechnya kuna suala zaidi ya kuipunguza Urusi nguvu. Chechnya ina mafuta. Jinginewe zaidi Mchechnya na Mrusi ni watu tofauti wenye dini, lugha, na tofauti zingine za kiutamaduni. Wahusika wakuu wa vita hivi ni Wachechnya wenyewe wakisaidiana zaidi na Waislamu toka nchi za Kiarabu.
Halafu kuhusu Museveni na ndege za kijeshi sina hakika nalo. Lakini sidhani kama katika maadili ya kivita kama anaruhusiwa kutumiwa ndege kupigana LRA.
Halafu suala la Dubai Ports World limesitishwa. Kwa hiyo bado hawajaanza utendaji. Nakuomba fuatilia tena au kama mimi ndiyo sina habari kamili naomba unijulishe.
Halafu unaposema Burundi vita imekwisha na kwamba kuna vikundi vidogo vidogo tu hiyo ina maana vita bado ipo. Sijui fasili nzuri ya vita kwa Kiswahili lakini kwa Kiingereza naweza kusema War is a fight for the gain based on right or wrong reason/s. Mwanamuziki Gill Scott-Heron katika wimbo wake Work for Peace anasema "..Peace is not absence of war. Peace is even the absence of rumours of war.." Kwa hiyo pasipo amani pana vita.
Nisikuchoshe sana bali nakuomba usome tena waaraka wangu. Niliposema Burundi, Uganda na Kongo wanaweza kuwa vichochoro vizuri sana kwa wenye nia ya kuleta mabaya nchini mwetu. Sikusema Burundi inaweza kupigana na Tanzania. Jinginewe tusijisahau sana tukafikiri sisi wakubwa sana. Mtanzania aliyempiga Idd Amin siyo Mtanzania wa leo. Mtanzania yule alikuwa na dhana ya Utanzania chini ya itikadi ya Ujamaa ambayo ilikuwa inamgusa kila sehemu ya maisha yake ya kila siku kuanzia gazeti la UHURU/MZALENDO na DAILY NEWS/SUNDAY NEWS, Idhaa ya Taifa, Biashara na External Service za Radio Tanzania Dar es Salaam. Usafiri wa KAMATA na yale ya mikoa CORETCO, MORETCO na mengineyo, UDA, Reli ya Kati na TAZARA. Wakati ule palikuwa na umoja wa Kitaifa miongoni mwa Watanzania sasa hivi umoja huo umelegea sana kwa sababu ya kutokuwa na itikadi wala sera za kitaifa ya kitaifa. Kuwajibika, Ukweli na Uwazi, Ari mpya, nguvu mpya, na kasi mpya siyo sera wala itikadi hizi ni kauli mbiu ambazo hazijengi uzalendo wala utaifa.
Mungu Ibariki Tanzania.
MK said...
Ni Vizuri ndugu F MtiMkubwa Tungaraza kusema ya kwamba inabidi tuwe na tahadhari ktk kutengeneza watu watakaoweza kuwa waasi kwa sababu za kisiasa, kijamii, na kiuchumi.
Ni kweli machafuko mengi yanatokana na sababu za kiuchumi, tofauti za kisiasa, dini, ukabila, rangi, kijamii n.k. lakini ni kwamba ktk baadhi ya hayo mambo tumejaribu kuyaondoa na kuyavunja ndani ya Tanzania, Kitu kilicho baki ni hiki kitu cha Zanzibar na jinsi baadhi ya vyama vinavyo tekeleza siasa zao nchini Tanzania.
Baadhi ya hivyo vyama vimeshaambiwa fika kuweza kuacha hizo siasa za machafuko (kuwa na mawazo ya vurugu).
Kuhusu Ukabila Baba wa Taifa JK Nyerere aliweza kuliondoa na kuweza kufanya kila mtanzania kujiona ni sawa na kuwezesha kiswahili kuwa lugha ya Taifa ktk ardhi ya Tanzania.
Kuhusu swala la Zanzibar Hon. JK ameweza kupewa ushauri wa juu na ndio maana umeona ya kwamba imeanzishwa wizara ya Union Affairs: Hon. Dr. Hussein Ali Mwinyi under Vice-President's Office itakayo weza kuliangalia hili Tatizo na kulimaliza mapema iwezekanavyo.
Kuhusu idadi kubwa ya Vijana wasikuwa na kazi hili ni kweli na kila mara uwa nalizungumzia nikiwa baadhi ya watu fulani, Lakini hii serikali ya awamu ya nne imeonyesha ya kwamba wanafuatilia hili swala na wanataka kutengeneza nafasi nyingi za kazi na ndio maana juzi juzi umesikia nafasi nyingi za kazi zimetangazwa ktk jeshi na Polisi pia nafasi nyingi zitatangazwa hapo baadae ktk sekta na mashirika ya umma.
Kuhusu swala la Museveni kununua ndege za kivita ni swala ambalo nina uhakika nalo. Hii Vita ni ndefu sana (Miaka 18)ambapo Joseph Kony anapata msaada toka Sudan, Pia vile vile nao Uganda wanawapa SPLA(Sudan People's Liberation Army)msaada kupigana na Serikali ya Sudan, Vile vile Joseph Kony anapata msaada toka DRC (The Democratic Republic of the Congo) ambapo Juzi juzi Museveni baada ya kushinda Uraisi ametangaza ya kwamba ataivamia tena DRC kwa kisingizio cha kuwafuata LRA na kupigana nao huko huko DRC. Pia LRA wanapata misaada toka mataifa mbali mbali ndani ya Africa na nje ya Africa.
Kwa habari za mwaka November 2002 nilizo nazo hii Vita imegharimu Serikali ya Uganda (UPDF) yafuatayo:
1: Matumizi ya jumla ya 367 million USA dollars kwa matumizi ya Kijeshi.
2: Uchumi kukosa pato la Taifa kutokana na Kilimo ambapo wamepata hasara ya 212 million USA dollars.
3: Kupungua kwa utalii na kukosesha hilo Taifa kiasi cha 185 million USA dollars.
4: Kuongezeka kwa gharama za uduma za matibabu kwa jumla ya 138 million USA dollars.
5: Raia wapatao 23, 520 wanakadiliwa kufa kutokana na Vita.
Na watu zaidi ya Million Moja kukosa makazi au kuama makazi yao ktk maeneo ya
Vita.
Maelfu ya kabila la Acholi kuweza kupata vilema vya maisha kutokana na hii Vita.
6: kutokana na hii report ya mwaka 2002 inasemekana, Kuendelea na hii Vita Uganda
itagharimiwa asilimia 10 ya GDP ya nchi yao. Pia October mwaka huo Serikali ya
Uganda ilikata asilimia 25 ya matumizi ya wizara zake zingine na kupeleka nguvu
ktk kudhamini hii vita.
Kuhusu Dubai Ports World hili swala lina utata ndio maana nilisema hapo juu bado linazungumziwa na Congress na Senate ambapo kiongozi wa juu wa white house amesema ya kwamba kunyimwa haki kwa Dubai Ports World kutapeleka "I think it sends a terrible signal to friends around the world, that it's OK for a company from one country to manage the port, but not a country that plays by the rules and has a good track record from another part of the world can't manage the port," Bush said. Akimaanisha ya kwamba kunyimwa haki kwa Dubai Ports World ni kumaanisha ya kwamba ni sawa kwa UK (P&O kabla ya kuuzwa)kufanya kazi ndani ya USA lakini sio kwa United Arab Emirates (Dubai Ports World mmiliki mpya wa P&O) ambapo sio haki, hivyo ni picha mbaya kwa USA kwenda kwa mataifa mengine na kutafanya mataifa mengi ya Arabs kuogopa kuwekeza ndani ya USA.
Congress na Senate inakataa hili swala kutokana Dubai Ports World ni mali ya United Arab Emirates na vile vile wanakataa hili swala kutokana na baadhi ya wale watekaji wa 9/11 ktk zile ndege walitoka United Arab Emirates (wawili ktk United Airlines Flight 175 --> Marwan al-Shehhi, alikuwa ndio pilot na group leader Umri: 23 na Fayez Rashid Ahmed Hassan Al Qadi Banihammad Umri: 28.) Soma hapa kidogo.
Pia kutokana na report ya 9/11 Commission na ya Justice Department zimeonesha kwamba wengi wa magaidi ya 9/11 yalipata pesa na misaada mingi toka ndani ya United Arab Emirates, Sasa wanaona kama hawa watu wakipewa haya majukukumu si ndio magaidi wataingia ktk ardhi ya USA.
Lakini kutokana na Ushauri wa Serikali ya United Arab Emirates imeshauri Dubai Ports World kujiondoa ktk harakati zake hizo za kutaka kufanya kazi ktk ports za New York, Newark, Philadelphia, Baltimore, Miami na New Orleans na tarehe 09/03/2006 Dubai Ports World imetoa tamko rasmi haitaki tena kufuatilia hili swala ingawa hili swala lilikuwa bado linazunguziwa ktk Congress na Senate
Mwisho, Majeshi yetu (Vyanzo vyetu vya Ulinzi) vina uzoefu mwingi wa kuzima mapinduzi na uzoefu wa kulinda amani pia tuna macho ya kuona maadui (wowote wale ktk ndani na nje ya nchi wawe waasi, wenye mawazo ya kuasi au vingine hii kwa kushirikiana na mataifa mbali mbali duniani.) sasa mambo haya yakitokea nina uhakika yatazimwa chini ya masaa 24 au kuzimwa kabla ya kutokea. Ninachosema hapa mueshimiwa F MtiMkubwa Tungaraza ninakijua kwa undani na kwa makini.
Nashukuru sana F MtiMkubwa Tungaraza kuweza kubadilisha habari kati yangu na wewe.
Nadhani sitokuwa nimewaudhi baadhi ya wasomaji wengine, Kama mtakuwa mmeudhika kwa yote nawaomba mniwie radhi.Ukweli utabaki ukweli.
F MtiMkubwa Tungaraza...MK,
Ninafurahi kubadilishan mawazo nawe. Ninafurahi kuwa una imani kubwa sana juu ya vyanzo vyetu vya ulinzi. Hapa nina maswali kadhaa "..Hivi kama kweli vyanzo vyetu vya ulinzi ni kiboko namna hiyo silaha wanazotumia majambazi zinaingiaje nchini? Pili, vinashindwaje kudhibiti matukio ya ujambazi, uingizaji na upitishaji wa madawa ya kulevya kwa mfano makonteina ya mihadarati yaliyokamatwa Romania, na utoroshaji mali kwa mfano makonteina ya mchanga wa dhahabu bandari ya Tanga.."
Halafu ajira katika jeshi, polisi, mashirika na makampuni zinahitaji qualifications za kitaaluma na jeshini na polisi pia wajihi. Tukumbuke kwamba mwekezaji Tanzania hajafungua makampuni yanayohitaji harubu(manual labour)! Kwa hiyo vijana wasiyo na elimu hawahitajiki kwenye uzalishaji mali na utoaji huduma. Wengi wa wawekezaji wamewekeza kwenye rasilimali za asilia kama madini, mbuga za wanyama, na huduma za jamii kama mabenki, mahoteli, usafiri wa anga, na majini. Ardhini hakuna mwekezaji atayejipinda kuwekeza kwenye usafiri wa mabasi au kukarabati na kuboresha huduma reli ya kati, sana sana wanaitamani reli ya TAZARA ambayo kwa mikataba yake hatuwezi kuibinafsisha. Hapa naomba unipe taarifa za kweli(facts) mpango/mipango ya/wa serikali wa kuboresha na kukuza ajira kwa vijana. Wiki iliyopita nilijibu ujumbe kutoka kwa jamaa yangu mmoja aliyeniuliza kuhusu "..mafanikio ya mpango wa maji safi kwa wote ifikapo mwaka 2000.." Ninatumaini hili suala la ajira kwa vijana halitakuwa kama la mpango wa maji safi kwa wote ifikapo 2000.
Kuhusu hali ya usalama Zanzibar hilo ni jambo linlohitaji mikakati ya kweli. Kwa sababu makovu na vidonda vya vilivyosababishwa wakati wa utawala wa sultani, machafuko na mauaji wakati wa uchaguzi wa mwaka 1963/4, mapinduzi ya Januari 1964, machafuko ya 1972 na mauaji ya Hayati Sheikh Abeid Aman Karume, machafuko na mauaji ya Januari 2000 makovu na madonda haya bado mabichi miongoni mwa Wazanzibari.
Mshairi maarufu wa Kiayalendi William Butler Yeats katika shairi lake la The Second Coming alisema
"...Turning and turning in the widening gyre
The falcon cannot hear the falconer;
Things fall apart; the centre cannont hold;
Mere anarchy is loosed upon the world,
The blood-dimmed tide is loosed, and everywhere
The ceremony of innocence is drowned;
The best lack all conviction, while the worst are full of passionate intesity.."
MK, the Second Coming yaweza kuja popote ulimwenguni. Watanzania kama wanaulimwengu wengine wowote hatuna sababu ya kufikiri kwamba Second Coming kwetu haiwezi kuja. Kuna msemo jihadhari kabla ya hatari ambapo kinyume cha msemo huo ni kwamba mwenziyo akinyolewa wewe tia maji. Watanzania tuna nafasi kubwa ya kuchagua kati ya jihadhari kabla ya hatari au mwenziyo akinyolewa wewe tia maji.
Mkweli kwa nchi yangu,
MK said... Ni kweli unayo sema muheshimiwa F MtiMkubwa Tungaraza, Silaha wanazotumia majambazi ktk nchi yetu ni baadhi ya Silaha chache zinazotoka nje ya nchi na hii inafahamika kwa baadhi ya wakubwa ndani ya jeshi na ndani ya Serikali yetu!! Kingine utakuta ata namba ya silaha iliyohusika ktk tukio la ujambazi inajulikana ni ya mmliki fulani au maganda ya silaha yanajulikana ni ya aina ya silaha fulani ambapo ndani ya nchi zinamilikiwa eidha na idadi fulani ya watu lakini kutokana na uozo ktk Jeshi fulani utakuta wanakaa kimya (kufumba macho).
Vyanzo vya ulinzi vya nchi hii ukiacha hilo jeshi wanafahamu hayo yote kuhusu silaha chache kutoka nje ya nchi ama baadhi ya watu kufumbiwa macho lakini mimi, wewe au mtu mwingine hauwezi kuingilia kati maana watakumaliza na kukuulia mbali na kuacha familia, ndugu, marafiki zako wakiteseka.
Hizo Silaha ni tishio kwa Raia na Taifa kwa ujumla lakini endapo idadi kubwa ya hizo Silaha (za kutishia mapinduzi) zingepitishwa ndani ya nchi basi hawa vigogo wala rushwa wangeingiliwa kati.
Mtu kuvamia Bank na kuondoka na Million 300 au zaidi sio kazi ya majambazi tu bali ni kazi ya kila Dirty cops na walinzi wa eneo husika au wafanyakazi wa eneo husika.
Hawa watu (Dirty cops) na hayo majambazi yanajulikana yalipo lakini kitu kinachoendelea ni kufichana. Unabidi uelewe ya kwamba kazi hii ya kulinda raia na mali zake ndani ya nchi ufanywa na jeshi lingine yaani kila kitengo kina kazi zake na mipaka yake sasa mfano kama afisa wa PCB au kitengo chochote (State Secret Service, military intelligence, Government Agencies n.k) akijua kwamba Kiongozi mmoja au Mkuu mmoja wa jeshi ni mla rushwa au anafanya Dirty games na aka-report kwa mkuu wake kisha akaambiwa kaa kimya na kupewa kitu kidogo (Pesa) unadhani utafanya nini? Naomba majibu!!
Lakini tumeona ya kwamba JMK ni mtu aliye serious na ndio maana unaona mabadiliko makubwa ndani ya hilo jeshi na ndani ya nchi kwa ujumla na wengine wakipoteza kazi zao au kuamishwa na ninakuadi ndugu F MtiMkubwa Tungaraza kuna mengi makubwa utayasikia labda wasiyaweke wazi kwa wananchi. Yaani watu wana ma-million mengi ya pesa ndani ya nchi na nje ya nchi na ata ukichukua mishahara yao na kuzidisha mara miaka mitano (5) hauwezi kufikia hiyo idadi ya pesa kweli inatisha!!
Mtandao huo wa ujambazi unao sema ni huo ambao unajulikana na kila mtu ktk vyanzo vya ulinzi lakini ni uzembe ktk hilo Jeshi, ndugu yangu wewe unadhani hawa watu hawajulikani? Wengine wanaishi kama Viongozi wa nchi na kulindwa!! Tumshukuru Hon. JMK na bwana Mwema watatuondolea uozo uliojaa ktk jeshi hilo.
Baada ya Serikali kuomba vyanzo vya ulinzi kutoa hiyo idadi ya majambazi na hao wasaidizi wao si umeona haijachukua muda kuweza kutolewa majina yao na wengine kukamatwa, kusimamishwa kazi, kubadilishwa sehemu za kazi, n.k
Muheshimiwa F MtiMkubwa Tungaraza nadhani wewe ni mtu mzima ambaye unaona mbali sana, Hii biashara ya madawa ya kulevya unadhani inafanywa na walala hoi? Hii inafanywa na The Big Bosses ambao wanatoa kickback nyingi na kubwa sana hili walindwe, lakini jalibu wewe na uone kana kwamba ujakamatwa siku hiyo hiyo.
Kuhusu mchanga wa dhahabu unashanga sasa hivi mbona hii ilikuwa siku nyingi enzi hizo ktk migodi yetu ya madini ndege zinabeba na kuondoka nayo, Hii inafahamika lakini ni tatizo za Administration kuweka sheria au kanuni zisizo eleweka. Unadhani mpaka sasa kiasi gani cha madini uondoka nchini na manufaa makubwa wanayapata wachache kuliko yule mlala hoi au mwananchi kwa ujumla aliye karibu na mgodi? Kuna kipindi nilipata habari kwamba bwana JMK na Serikali yake watapitia Contracts zote za haya makampuni na mengine ili kujua kama wananchi na Taifa linapata mazuri yoyote yale sasa sijajua kunaendeleaje!!
Kwa ujumla yote yanajulikana lakini huu ni ule uzembe wa baadhi ya Viongozi wa Africa.Na wakati huo huo ingawa kuna hawa Dirty Cops na Viongozi wazembe pia kuna idadi kubwa ya wana-usalama ndani na nje ya nchi walio wasafi na kufanya kazi kwa bidii ktk kila siku ya Mungu na kulinda Taifa na wananchi wa nchi hii 365/24/7.Pia naomba ipe muda hii serikali ya awamu ya nne na utaona ule uozo unao fanya wote tuonekane tumeoza ukiondolewa.
Kuhusu Investors ni swala zuri sana la kuangalia tukitaka kuweza kushindana na mataifa mengine ktk uchumi wa nchi. Hii inabidi kwa Serios Investors kukaribishwa toka kila pembe ya dunia na kuja kuwekeza nchini kwetu na pia inabidi tuwaangalia wale watakao kuwa wapo tayali kufanya biashara kwa muda mrefu na kila Contracts zitazo ingiwa inabidi ziwe na manufaa kwa taifa na wananchi.
Kingine sio tu kukaribisha wawekezaji bali tunabidi kutoa elimu mbali mbali kwa kila mwananchi maana hakuna mwekezaji atakaye kuja na kuwekeza alafu hakuna wafanyakazi!! Unadhani atakubali kuajiri mtu toka nje ya nchi? Kwanini afanye hivyo? Yeye anataka watu toka nchi husika ili aweze kupunguza costs!! Tatizo hapa hakuna msingi maradufu wa elimu wa kuwezesha watoto wetu kwenda kusoma na hii inachangiwa na umasikini na matatizo mengi sana, Leo hii kama mtoto hajafaulu na kwenda shule ya serikali basi kusoma kumekwisha maana mzazi atatoa wapi pesa (Malaki) kumpeleka mtoto kusoma? Sio ndio inabaki kuamua kumuozesha kama akiwa mwanamke? Kama mwanaume anabaki kuwa mkulima au kuoa!!
Kama Taifa hili linataka kuendelea ktk maisha ya sasa na ya baadae inabidi tuwekeze kwa watoto wetu, Matumizi ya Serikali kudhibitiwa, Tuache rushwa, wizi na ubinafsi kwa Viongozi na wananchi kuangalia familia zao tu na kujilimbikizia utajili mkubwa na kuiba mali za umma au mahali husika afanyapo kazi.Pia tuache uzembe na kufanya kazi kwa bidii.
Mataifa yaliyo endelea ni kutokana ni kwamba raia wote wamesoma na kuelimika na kila mtu ana professional yake.Na gharama za elimu kwa wazawa zinakuwa ni za bei ya chini na sio haya malaki ambapo ni wachache wanao soma hizo shule!! Baada ya kila mtu kuwa na professional yake wote ufanya kazi kwa bidii bila kuibia Taifa na wanakuwa kweli wasafi kila kona ktk kazi zao maana wao ufikiria je kizazi kijacho kitapata manufaa gani? Na ndio hapo wote ufanya kazi kwa manufaa ya Taifa na wananchi!!
Kingine kwa watanzania wengi walio nje ya nchi wakifika hapo walipo wanashindwa kujiendeleza ki-elimu ili kesho na kesho kutwa Taifa liwe na idadi kubwa ya wasomi, Nafahamu maisha ni magumu kwa watanzania walio wengi wa nje lakini ni lazima wakumbuke vitu viwili yaani Pesa na elimu!!
Sasa kama tukiwezesha Raia wetu kusoma na kupata ujuzi wawekezaji watakuja kuwekeza tu na pia Serikali iweke taratibu za kuitangaza Taifa letu kwa zaidi kama mataifa mengine ufanya.Tuchukue advantage kwa Taifa letu kuwa nchi ya Amani maana wawekezaji siku zote uenda mahali penye Amani sasa ni wakati kwa Serikali kuwakaribisha.
Kingine tunabidi tutafute suluhisho la umeme maana nina sikia ya kwamba nyumbani siku hizi hakuna umeme!! Sasa mwekezaji yoyote siku zote atakuja kama kuna bara bara nzuri, mawasiliano mazuri (simu na mawasiliano ya technogy zote, n.k) au kuna umeme wa kuwezesha kufanya production.
Kingine mimi ninashangaa utakuta hizi wizara zipo ktk safari za nje kila siku au Taifa letu lina barozi kila kona ya dunia lakini sijui zinafanya nini? Kwanini wasiweze kutumia mwanya wa hizo safari au huko mahali walipo kuitangaza Taifa na kutafuta wawekazaji walio serious na wa maana wenye capital kubwa ili waje kuwekeza? Kwasababu hakuna maana ya kufunga safari wizara karibia zote kwenda nje kama show ambapo wakirudi Taifa limepoteza mamillion ya Pesa na hakuna la maana linalopatikana na mwananchi wa chini anabaki kuumia na kodi au kulipa madeni ya Taifa!!
Yaani nina uchungu na hili Taifa na wananchi wake hii ni kwasababu ninajua kila kitu kinachofanywa.Nina uchungu kuona watu wanazidi kuteseka kila kukicha na maisha yao hayabadiliki na hii hali ulithiwa toka kwa Babu, Baba hadi watoto lakini wachache ndio wenye maisha ya kifahali.Kama kweli hii nguvu ya JMK itaendelea siku zote basi nadhani tutafanikiwa.Kwa hasira hii niliyo nayo yaani ninaweza kuandika mpaka ukurasa huu ujae lakini naomba niishie hapa kwa leo.
Mwisho, vyanzo vyetu vya ulinzi vina macho makubwa sana na hiyo mifano uliyo sema inajulikana lakini ni uzembe na matamanio ya baadhi Viongozi wa Askari wa juu kushirikiano na hao waharifu.Lakini endapo machafuko au mtu au Taifa lingine likiwa na mawazo ya kufanya mapinduzi au uasi nina uhakika yatazimwa chini ya masaa 24 na hii ndio udhibitisho. Naomba fanya uchunguzi maana siwezi kusema mengi ktk Internet na hapa nimejalibu kudodosa tu kwakuwa natumia MK aka The pretender.
Nadhani sitokuwa nimewaudhi baadhi ya wasomaji wengine, Kama mtakuwa mmeudhika kwa yote nawaomba mniwie radhi.Ukweli utabaki ukweli.