Hivi kama ukoloni usingekuja Afrika, Afrika ingekuwa wapi leo?
Nina amini watu tumeumbwa na uwezo tofauti ili kutimiza malengo tofauti tofauti.
Ninaamini hakuna mtu ameumbwa kumfuatiza mwingine awe kipimo cha kuendelea kwake.
Ninaamini katika kila mtu kujiangalia mwenyewe na alichonacho na jinsi gani anaweza kukitumia ili kubadilisha maisha na mazingira yake.
Hivi kwa mtindo wa kujipima maendeleo kwa vipaji vya wengine tunadhani kuna siku tutakuja kuwa DUNIA YA KWANZA....???
Bado najiuliza, kama ukoloni usingekuja Afrika, labda tungekuwa tumegundua mambo meeengi ya sampuli nyingine tofauti na ya kimagharibi...
NIKO MAWAZONI...!!
Da' Mija na wanawake wa shoka..
16 May 2013
08 May 2013
03 May 2013
SHUKRANI..
Watanzania
waishio New jersey na New York tunapenda kutoa shukurani zetu za dhati
kwa ushirikiano wenu mkubwa mlio tuonyesha katika kipindi hiki kigumu.
Kwa ajili ya blog za watanzania tuliweza kufikisha habari za msiba wa
marehemu Adolf aka Brian aka Thadeo Lwakajende kwa watu wengi sana kwa
muda mfupi sana kuliko tulivyotegemea. Kwa ushirikiano wenu huo tuliweza
kufanikiwa na kuweza kukamilisha shughuli hii kwa kipindi kifupi sana
kuliko tulivyokua tunafikiria.
Adolf alipelekwa kulazwa katika nyumba yake ya milele jana
Jumatano May 1st, 2013 huko katika makaburi ya Mt Pleasant, Hawthorne,
NY 10532 | Reactions: |
28 April 2013
MSIBA NEW JERSEY....
Kuna kijana amefariki New Jersey, USA. Kijana
aliyefariki alinajulikana kwa jina la Adolf, Brian au Tadeous
Rwekagende. Alikua anasema alisoma Tambaza na alikua na mdogo wake
anaitwa Rodrick Rwekagende ambaye naye alikua anaishi Texas. Ila cha
kusikitisha ni kuwa huyo mdogo wake alisema alifariki mwaka jana mwezi
wa nne (Tanzania).
Adolf alikua anasema baba yake na mama yake walifariki yeye na mdogo wake huyo wakiwa wadogo. Sasa yeye alikulia kwa mjomba wake. Juzi Adolf alipata massive stroke na kulazwa st Barnabas hospital, Livingston, NJ na kufariki. Mpaka sasa hivi kuna watu wametafuta ndugu zake na kumpata mjomba wake mmoja huko Bukoba vijijini. Hatukuweza kupata ndugu wa karibu hapa marekani na mpaka sasa hivi maiti yake ipo hospital haijawa claimed. Hivyo kama binadamu tumeamua kujichangisha ili tuweze kupeleka mwili wa mwezetu Tanzania kwa mazishi. Gharama za kuzika huku na kusafirisha kupeleka Tanzania ni karibu sawasawa tu hivyo tunaona ni bora akapumzike na ndugu zake Tanzania.
Hivyo tunaomba mtupostie kwenye blog zenu hili tangazo liwafikie watanzania watakaopenda kumsaidia ili apelekwe Tanzania tutashukuru sana. Tumefungua mahali pa kuchangisha hela http://www.donationto.com/adolfsendhomecost au kama mtu anatumia paypal account ni adolffuneralcost@gmail.com. Tutawapa majina ya watu watakaokua kwenye kamati ya kukusanya hela mara tutakapomaliza kikao tunachotegemea kufanyika Jumamosi. na hela zote zitaonyeshwa zilivyotumika kama zipo extra zitapelekwa huko kwa wajomba zake Bukoba.
Na kama kuna mtu ana picha yake basi mtutumie kwa sababu hakuna mtu aliye na picha yake. ID yake ipo hospital hawawezi kumpa mtu mpaka wakishajua nani anachukua mwili na mahali alipokua anaishi hawaruhusu mtu kuingia kwa sasa mpaka wakishajua mazishi ni wapi au ndugu wa karibu ni wapi. Hivyo hamna mtu ana picha yake..
Please sisi hapa tunajitahidi ili azikwe kama ubinadamu hivyo huu sio muda wa kuanza kuuliza maswali kwa nini hiki wala kile...Kwa vile hata sisi tuna maswali mengi na hakuna mtu mweye jibu....Tunachojua ni kuwa alipata massive stroke na amefariki na hakuna ndugu yake wa karibu huku marekani.
Tunatanguliza shukurani na pia kama blog yako hupost mambo ya habari tunaomba utusaidie kuforward hii email kwa watu wengine...Kuna wazee wako NY kama wakikukubali kushughulikia huu msiba tutawatangazia na kuwapa information mpya. Na hela zitakazopatikana zitahamishiwa kwenye fund yeyote watakayofungua kama wataamua kufungua mpya au wataamua kuendelea na hi hii. Tunachotaka ni kusafirisha kijana wa watu Tanzania kwa sababu sasa hivi hilo ndio lengo letu....na hakuna mtu yeyote aliyesema kitu chochote hivyo kama kikao kikifanyika basi tutawaeleza linaloendelea.
Nitajitahidi kuupdate kinachoendelea katika twitter handle yangu @swahilimom
Regards,
Pauline........................
Adolf alikua anasema baba yake na mama yake walifariki yeye na mdogo wake huyo wakiwa wadogo. Sasa yeye alikulia kwa mjomba wake. Juzi Adolf alipata massive stroke na kulazwa st Barnabas hospital, Livingston, NJ na kufariki. Mpaka sasa hivi kuna watu wametafuta ndugu zake na kumpata mjomba wake mmoja huko Bukoba vijijini. Hatukuweza kupata ndugu wa karibu hapa marekani na mpaka sasa hivi maiti yake ipo hospital haijawa claimed. Hivyo kama binadamu tumeamua kujichangisha ili tuweze kupeleka mwili wa mwezetu Tanzania kwa mazishi. Gharama za kuzika huku na kusafirisha kupeleka Tanzania ni karibu sawasawa tu hivyo tunaona ni bora akapumzike na ndugu zake Tanzania.
Hivyo tunaomba mtupostie kwenye blog zenu hili tangazo liwafikie watanzania watakaopenda kumsaidia ili apelekwe Tanzania tutashukuru sana. Tumefungua mahali pa kuchangisha hela http://www.donationto.com/adolfsendhomecost au kama mtu anatumia paypal account ni adolffuneralcost@gmail.com. Tutawapa majina ya watu watakaokua kwenye kamati ya kukusanya hela mara tutakapomaliza kikao tunachotegemea kufanyika Jumamosi. na hela zote zitaonyeshwa zilivyotumika kama zipo extra zitapelekwa huko kwa wajomba zake Bukoba.
Na kama kuna mtu ana picha yake basi mtutumie kwa sababu hakuna mtu aliye na picha yake. ID yake ipo hospital hawawezi kumpa mtu mpaka wakishajua nani anachukua mwili na mahali alipokua anaishi hawaruhusu mtu kuingia kwa sasa mpaka wakishajua mazishi ni wapi au ndugu wa karibu ni wapi. Hivyo hamna mtu ana picha yake..
Please sisi hapa tunajitahidi ili azikwe kama ubinadamu hivyo huu sio muda wa kuanza kuuliza maswali kwa nini hiki wala kile...Kwa vile hata sisi tuna maswali mengi na hakuna mtu mweye jibu....Tunachojua ni kuwa alipata massive stroke na amefariki na hakuna ndugu yake wa karibu huku marekani.
Tunatanguliza shukurani na pia kama blog yako hupost mambo ya habari tunaomba utusaidie kuforward hii email kwa watu wengine...Kuna wazee wako NY kama wakikukubali kushughulikia huu msiba tutawatangazia na kuwapa information mpya. Na hela zitakazopatikana zitahamishiwa kwenye fund yeyote watakayofungua kama wataamua kufungua mpya au wataamua kuendelea na hi hii. Tunachotaka ni kusafirisha kijana wa watu Tanzania kwa sababu sasa hivi hilo ndio lengo letu....na hakuna mtu yeyote aliyesema kitu chochote hivyo kama kikao kikifanyika basi tutawaeleza linaloendelea.
Nitajitahidi kuupdate kinachoendelea katika twitter handle yangu @swahilimom
Regards,
Pauline........................
| Reactions: |
27 April 2013
Happy Birthday Da' Mija...
Nina kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kunilinda, kunibariki, na kunipa yote ayahitajio binadamu katika maisha yake. Mungu ni mwema na leo nimeanza maisha rasmi.
Ninawashukuruni sana wadau wangu wote, kwani kwa njia moja au nyingine mmenisaidia kufika hapa nilipo. Asanteni sana.
Happy Birthday Da' Mija.
| Reactions: |
25 April 2013
Mwanamke wa Leo: Caster Semenya..!!
| Reactions: |
22 April 2013
Kutoa mimba (Abortion) ni wazo zuri au la kijinga?
Suala la kutoa mimba kwa makusudi limekuwa likiongelewa katika mijadala mingi duniani, na hadi leo hii bado kuna mvutano juu ya uhalali wake.
Nami leo nimeona niulete mjadala huu ili tujadiliane na kuangalia ni kwa kiwango gani jamii yetu ina nufaika au kutonufaika na utoaji mimba...
Karibuni jamvini...
| Reactions: |
21 April 2013
Yesu anaponya... Angalia muujiza Live..!!
Jumapili njema..!!
| Reactions: |
19 April 2013
Salaam za Rambirambi Bi Kidude..
“
Baraza limestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa ya kifo hiki cha Bi
Kidude ambaye mchango wake katika muziki wa taraab ni mkubwa mno na unahitajika sana, pengo aliloliacha ni kubwa
kwani ubunifu wake bado unahitajika katika tasnia hii.” Baraza linatoa pole kwa
familia ya marehemu na wasanii wote nchini, aidha tunawatakia moyo wa subira
katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na mpendwa wetu.
Mwenyezi
Mungu aipumzishe mahala pema peponi roho ya marehemu. Baraza liko pamoja na
familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.
Imetolewa
na
Godfrey
Mngereza
Kaimu
Katibu Mtendaji
Baraza
la Sanaa la taifa.
| Reactions: |
18 April 2013
Neno la kumalizia siku !!
If you want to stand out, don't be different, be outstanding.
Meredith West.
Meredith West.
| Reactions: |
17 April 2013
16 April 2013
15 April 2013
Kelvin Doe!! Haijalishi umezaliwa wapi mtu kuwa na akili..!!.
Hivi ingekuwaje kama watu tungejaribu kutumia hata nusu ya uwezo tulionao kuleta mabadiliko? Kelvin amenitia moyo sana!!
| Reactions: |
12 April 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)











