11 November 2005

Ellen Johnson-Sirleaf ....Mwanamke wa shoka.

Naam, Ellen Johnson Sirleaf ameibuka mshindi katika kinyang'anyiro cha kiti cha urais nchini Liberia juma hili. Mwanamama huyu ambaye atakuwa rais wa kwanza mwanamke barani Afrika, alikuwa akichuana na Kijana machachali mwanakandanda wa zamani George Weah. Hongera sana Mama.

2 Comments:

At Sunday 13 November 2005 at 01:53:00 GMT, Blogger mwandani said...

Hongera mama sirleaf, utawala wa nchi hiyo unarudi kwa wale wale Americo-Liberians... wazawa wa makabila mengine, akina doe waliburunga...
Huyu mama alikuwa karibu sana na Taylor... hebu tumuangalie mitikasi yake.

 
At Monday 14 November 2005 at 08:12:00 GMT, Blogger Egidio Ndabagoye said...

Mwandani kweli huyu mama Sirleaf alikuwa karibu sana na Bw Taylor.Kwa hiyo katika utawala wa Mama huyu kuna uwezekano mkono wa Bwa Taylor ukawepo.

 

Post a Comment

<< Home