17 October 2005

MtiMkubwa!!!!!!!

F.T kijana machachali sana, ni yule aliyeleta hoja ya "binadamu ni sawa lakini si sawasawa" nenda hapa utafute aliyosema,kwa wale waliobahatika kukumbana naye watakubaliana nami. Mara yangu ya kwanza kumsikia ilikuwa miaka 12 iliyopita pale chuoni sanaa bagamoyo, ndio kwanza nilikuwa naanza chuo. Basi ile kutua tu, tukapata stori...bwana...bwana ...alikuwepo Fide Tungaraza hapa chuoni....na sisi tuko enhe..., wakuda wakaendelea.... bwana sijui kama tutakujapata msanii kama yule..., jamaa hatari sana yule, kwanza korofi, pili limejaaliwa kichwani, tatu jukwaani kama hakupanda basi watazamaji watatoka wakilalamika.....,iko siku alitoa kituko jukwaani ilibidi mchezo usimame kwa muda kwani wahusika walishindwa kuhimili na wote kuangua kicheko kosa ambalo ni kubwa sana jukwaani (kutoka nje ya husika yako), lakini siku hiyo hata mwalimu alisamehe kosa. Basi hayo ni machache tu ya huyu bwana Tungaraza.

Turudi katika nilichotaka kukizungumzia leo, ni hili jina lake lingine la "Mti mkubwa". Binafsi ni juma lililopita ndio nimejua kuwa ana jina jipya la Mti mkubwa.
Nililitizama hili jina..., nikamtizama na mtu mwenyewe, nikawa sipati maana hasa ya chanzo chake, nikaona nimwandikie nimuulize...

Mti mkubwa hivi jina hili la Mti mkubwa chanzo chake ni nini hasa??

Jibu alilonipa nimeona nisilifaidi peke yangu, hili hapa chini:

BIBIE JINA LA MTI MKUBWA NILIPEWA KWA SABABU YA WASIFU WAKE:

1. Kuwa na matawi mengi, mtimkubwa mrefu sana kwamba ukifika kileleni kwangu
utaona mengi kwa upeo wa mbali.

2. Nina shina pana hivyo huwezi kunikwea kwa hiyo lazima unipande.

3. Shina hili pana ukitaka kulikata ni lazima uwe na vifaa madhubuti, vinginevyo
utakuwa unajisumbua na kupoteza nguvu zako bure.

4. Shina hili pana huwezi kulifumbata wala kulikumbatia kwa hiyo lishike
unapofikia,
usipofikia paache kama palivyo.

5. Mti mkumbwa una mizizi mirefu huwezi kuning'oa kiurahisi, mizizi yangu
imejikita
kinani sana kwa hiyo siyumbishwi wala kuangushwa na upepo wala vimbunga.

6. Majani mapana ya mtimkubwa mazuri kwa kivuli, watu wengi huja kujipumzisha
chini ya mtimkubwa, mtimkubwa nyumba vijidudu vidogovidogo, majoka ya namna kwa
namna na ndege wenye rangi na sauti nzuri.

7. MtiMkubwa huu hauzai matunda yaliwayo lakini hata ukiyala si sumu hayakuui.

Haya sifa hizo ndio chanzo cha U-MtiMkubwa kwa kaka yetu. Hii sifa ya saba hii, akili yangu inaniambia ni fumbo la imani, tungependa aifafanue kidogo.

Udumu MtiMkubwa, tutajifunza mengi kutokana na sifa hizo.

4 Comments:

At Monday 17 October 2005 at 10:25:00 BST, Anonymous Anonymous said...

This comment has been removed by a blog administrator.

 
At Wednesday 19 October 2005 at 09:01:00 BST, Blogger Ndesanjo Macha said...

Fide, Fide, Fide...hummalizi. Najilaumu sikupata muda wa kutosha kuketi naye pale Helsinki. Nadhani Fide ndiye anayesubiriwa sasa kwenye ulimwengu wa blogu.

 
At Wednesday 19 October 2005 at 09:52:00 BST, Anonymous Anonymous said...

This comment has been removed by a blog administrator.

 
At Wednesday 19 October 2005 at 09:54:00 BST, Blogger Mija Shija Sayi said...

Tuendelee kumpigia kelele, iko siku atazichoka na kuamua kutunyamazisha.

 

Post a Comment

<< Home