16 September 2005

Mbona tunamuacha peke yake??

Kina mama sasa sijui hata tunataka nini, tumelia sana juu ya usawa wa jinsia,tuwe na haki sawa na wanaume, nasi tutambuliwe na kuthaminiwa kama wanaume. Yote tumeyapata sasa kijasho chembamba kinaanza kututoka, tunaogopa nyadhifa za juu hususani uongozi wa nchi, suala la kutokujiamini linarudi palepale. Sawa yote tisa...kumi...basi hata mmoja wetu anapojitokeza tunashindwa hata kumuunga mkono!!! loooh kazi bado tunayo. Dunga hapa ujisomee mwenyewe.

1 Comments:

At Sunday 2 October 2005 at 15:26:00 BST, Blogger Ndesanjo Macha said...

Watu husema eti adui wako mkubwa ni wewe mwenyewe. Adui mkubwa wa masikini ni masikini mwenzie, adui mkubwa wa mwafrika ni mwafrika mwenzie, adui mkubwa wa mwanamke ni mwanamke mwenzie...sijui kama tunaweza kusema kuwa hali huwa hivi kila mara, ila kuna ukweli fulani...

 

Post a Comment

<< Home