12 May 2005

Utukutu wa chama.

1. Chama chetu kimetuongoza, hadi uhuru tulipoupata,
Kinaendelea kuongoza, kufikia lengo umoja,
Mwenyekiti Mwalimu Nyerere, mwenye hekima na wingi wa sifa,
W: Tanzania.

Ewe chama chombo chetu madhubuti kabisa,
Ndio wewe nguzo, muokozi wa taifa,
Mwenyekiti Mwalimu Nyerere mwenye hekima na wingi wa sifa,
W: Tanzania.

2. Kwa wasafiri wenye busara, ni wajibu wao kukumbuka,
Wafikapo safari salama, hata njiani bado wakiwa,
Kulinda chombo chao vyema, pia nahodha kumshikilia,
W: Tanzania

3. Ulifika wakati mgumu, wananchi walifadhaika,
Utumwa ukoloni ni sumu, sisi sote tulihangaika,
Ni wajibu wetu kushukuru, Nyerere alipojitokeza,
W: Tanzania.

4. Chama chetu kweli ni ngome ya chuma, sisi sote tunazingatia,
Mwalimukiongozi wa umma, nani twaweza kumlinganisha?
Ametutoa katika utumwa, wananchi sasa tnalinga.
W: Tanzania.

NCHI YANGU ENZI HIZO...

4 Comments:

At Thursday 12 May 2005 at 22:54:00 BST, Blogger Indya Nkya said...

Sasa ondoa hilo neno utukufu weka "utukutu" wa chama.

 
At Friday 13 May 2005 at 08:15:00 BST, Anonymous Anonymous said...

ulicheza halaiki we?

 
At Saturday 14 May 2005 at 14:24:00 BST, Anonymous Anonymous said...

kweli umekuwa "malenga" wetu sasa!

 
At Sunday 15 May 2005 at 08:04:00 BST, Blogger Rama Msangi said...

kwakweli kama alivyosema Indya, hakika unatakiwa kusahau kabisa matumizi ya hilo neno Utukufu maana umebaki Utukutu hivi sasa

 

Post a Comment

<< Home